MAKING CHUNYA A HOTBED OF INNOVATION & INDUSTRIAL REVOLUTION
Search This Blog
TANZANITE CITY: The Africa's Factory & Innovation Powerhouse!
Tuesday, October 17, 2017
Tanzanite City Chunya Full Council Briefing Part 4
Sehemu ya nne ya mkutano wa utambulisho wa Tanzanite City kwa wakuu wa idara na madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Chunya ambako ndiko jiji linajengwa.
Sunday, October 15, 2017
Tanzanite City Chunya Full Council Briefing Part 3
Sehemu ya tatu ya mkutano wa utambulisho wa Tanzanite City kwa wakuu wa idara na madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Chunya ambako ndiko jiji linajengwa.
Saturday, October 14, 2017
TANZANITE CITY; FURSA MPYA NA MBEYA MPYA, KUELEKEA TANZANIA YA VIWANDA
Mpango wa ujenzi wa jiji la sayansi, teknolojia na
ubunifu katika wilaya ya Chunya mkoani
Mbeya unatoa fursa nyingine ya kiuchumi kwa watanzania na wakaazi wa mkoa wa
Mbeya. Katika wakati ambapo nchi yetu
ipo kwenye kipindi cha mpito kuelekea uchumi wa kati na wa viwanda, mkoa wa
Mbeya chini ya uongozi wa Mh. Amosi Makalla kwa kushirikiana kampuni ya ESTA-TZ
na uongozi mzima wa wilaya na halmashauri ya wilaya ya Chunya umeanzisha mpango
maalum wa kuifanya Mbeya kuwa kitovu cha maendeleo ya teknolojia na mapinduzi ya
viwanda katika bara letu la Africa kusini mwa jangwa la sahara.
Katika mpango huu ambao eneo la kuanzia, kiasi cha
kilomita za mraba miatano (500sqKm) katika wilaya ya Chunya, litatumika kujenga
jiji la Tanzanite. Lengo kuu likiwa ni kuondoa utegemezi wa taifa letu kwa
bidhaa na teknolojia mabalilmbali toka nje ya nchi. Katika kipindi cha miaka
kumi na tano ijayo Tanzanite city inatarajiwa kujenga uwezo wa taifa letu
katika ubunifu wa teknolojia na uzalishaji wa viwandani.
Ili kufikia lengo ambalo mkoa wa Mbeya umejiwekea kufikia
mwaka 2030, mkakati mahsusi umewekwa wa kuwekeza kwa Vijana wenye vipaji
wanaohitimu kutoka katika taasisi zetu za elimu ya juu. Pindi wanapohitimu masomo yao, Vijana hao watakuwa
wanawekwa kwenye makambi maalumu ya teknlolojia ndani ya jiji la Tanzanite,
ambako huko watapewa kila kitu wanachohitaji kuweza kujenge uwezo katika
masuala ya ubunifu wa teknolojia na uzalishaji. Vijana hawa watakuwa wanapatiwa
mafunzo maalumu ya kuwawezesha kuanzisha na kuendeleza viwanda vitakavyotokana
na kazi za kibunifu watakazokuwa wanazifanya makambini.
Mpango huu utawawezesha wazawa wote bila kujali mazingira
wanayotoka au asili ya mtu, kuweza kumiliki viwanda kwa pamoja na vijana
wabunifu ambao ndiyo watakuwa wakurugenzi wa makampuni hayo yatakayoundwa. Hadi
sasa kuna maeneo zaidi ya mia tatu (300 Technology development missions) ambayo
yapo tayari kuanza kufanyiwa kazi na vijana pindi ujenzi wa awali wa miundo
mbinu muhimu utakapokamilika. Inatarajiwa kwamba maandalizi ya awali ya ujenzi
wa Tanzanite City yatakamilika mwishoni mwa robo ya kwanza mwakani (March 2018)
ambapo jiji litaanza rasmi shughuli zake.
Miezi sita baadaye viwanda visivyopungua 60 vitaanzishwa
na kutoa ajira za moja kwa moja kiasi cha 1200. Baada ya hapo kila wiki
kutakuwa na viwanda vipya vinaanzishwa na idadi yake itakuwa ikiongezeka siku
hadi siku ambapo katika miaka 15 hadi 2030 jumla makmpuni 54,600 yanatarajiwa kuanzishwa na kutoa ajira
za moja kwa moja zisozopungua milioni mbili na nusu.
Tafiti zinaonyesha kuwa kila ajira moja rasmi inazalisha
ajira kati ya tatu hadi tano zisizokuwa rasmi. Hivyo katika kipindi cha miaka
kumi na tano ijayo Tanzanite City itaweza kuzalisha ajira kwa watu wanaokaribia
milioni saba. Sehemu kubwa ya watu hawa pamoja na familia zao watakuwa wanaishi
ndani ya wilaya ya Chunya na maeneo jirani katika mikoa ya Songwe na Mbeya. Idadi
hii ya watu itahitaji miundombinu mbalimbali ambayo Tanzanite City imejiandaa
kikamilifu kuijenga kwa kushirikiana na marafiki pamoja na wadau wetu wote wa
maendeleo katika mkoa wa Mbeya.
Tanzanite City inaleta fursa ya kipekee kwa wakazi wa Mbeya,
na watanzania wote kwa ujumla, kwani kupitia klabu ya marafiki wa Tanzanite
City kila mwanzanchi Mtanzania ataweza kushiriki kwa namna moja au nyingine
katika kujenga uchumi wa viwanda. Lakini pia kupitia klabu ya marafiki wa
Tanzanite City, watoto wa watanzania masikini wataweza kupata fursa ya kutumia
vipaji vyao kubuni teknolojia na kuanzisha makampuni watakayoyamiliki kwa
pamoja na watanzania wengine ambao pia ni wanachama wa klabu. Jambo hili
lisingewezekana bila ya Tanzanite City. Kwa utaratibu huu hakuna mtanzania
atakayeachwa nje ya uchumi wa viwanda kama atakuwa mwanachama wa klabu isipokuwa
kwa mapenzi yake mwenyewe!
Klabu ya marafiki wa Tanzanite City ni chombo muhimu sana
kwa ujenzi wa jiji la Tanzanite na uchumi wa viwanda kama tunavyotaka kwa
sababu kuu mbilli; moja ni kuwa, klabu ndiyo njia pekee ya uhakika
itakayowaunganisha watanzania wote na kuwapatia fursa ya kushiriki kikamilifu
katika ujenzi wa Tanzania ya viwanda kama wadau na wamiliki. Pili, klabu
kupitia michango na ada za wanachama ni chanzo muhimu cha mapato
yatakayowezesha kugharimia shughuli na miradi mbalimbali ya ujenzi wa jiji na
uendelezaji teknolojia. Wananchi kupitia klabu watafaidika na fursa nyingi sana
zitakazotokana na ujenzi wa jiji hili hasa katika maeneo ya miundombinu, na
huduma.
Kwa kuzingatia kuwa jiji la Tanzanite litakuwa kiwanda na
kitovu cha mapinduzi ya viwanda na maendeleo ya teknlojia katika ukanda huu wa
maziwa makuu ya Afrika, watu kutoka mataifa mbalimbali ya afrika watakuja Mbeya
aidha kama watalii, wawekezaji ama wafanya biashara, hivyo kupelekea kuwa na fursa
nyingi sana, baadhi nimeziorodhesha hapa:
1.
Huduma;
Usafiri na usafirishaji
wa watu na mizigo, huduma za hoteli na mikahawa, huduma za afya, elimu ya
msingi, secondary na vyuo (mahitaji ya vyuo ni makubwa kiasi cha kuhitajika
vyuo zaidi 16 vitavyo toa kozi maalumu zinazoendana na mahitaji ya shughuli za
Tanzanite City), ukusanyaji wa taka ngumu, huduma za ulinzi na usalama, huduma za
simu na data, n.k.
2.
Miundombinu
Ujenzi wa
barabara, mitandao ya maji safi na maji taka, uzalishaji na usambazaji wa umeme,
mawasiliano, n.k.
3.
Ujenzi wa nyumba
Nyumba za
kuishi, majengo ya biashara, ofisi na viwanda
4.
Biashara
Bima, mabenki,
maduka makubwa (Malls), wasambazaji wa bidhaa zinazozalishwa ndani ya jiji, wauzaji
wa bidhaa kwa matumizi ya nyumbani kama vyakula na vifaa vingine, sehemu za
burudani, n.k.
Ili mtu aweze kunufaika na fursa hizo, ni sharti awe
mwanachama wa klabu ya marafiki wa Tanzanite City, kwa maana nyingine anatakiwa
kuwa RAFIKI wa Tanzanite City. Rafiki wa kweli ni mtu ambaye yupo tayari
kujitoa kwa kila hali kwa ajili ya manufaa ya rafiki yake hata kama yeye
mwenyewe hafaidiki moja kwa moja na kujitoa huko. Marafiki wa Tanzaite City
watakuwa tayari kuichangia Tanzanite City kwa kulipia ada zao za uwanachama kwa
wakati ili kuwawezesha vijana wa watanzania kutimiza ndoto zao na kuigeuza
dunia kuwa wanachotaka. Kupitia klabu hii siyo lazima kuwa kila utakachochangia
lazima kikunufaishe, mchango wako utakuwezesha kuwa miongoni mwa wadau
watakoweza kunufaika na fursa ambazo michango yanu kama marafiki itakuwa
imetumika kuzitengeneza kupita vijana wetu wenye vipaji watakaokuwa makambini.
Ni wazi kuwa sasa wanachi wa mkoa wa Mbeya na watanzania
wangine wote tunapaswa kumuunga mkono mkuu wa mkoa Mh. Amosi Makalla, mkuu wa
wilaya na uongozi mzima
wa halmashauri ya wilaya ya Chunya, kwa kujiunga na klabu ya marafiki wa
Tanzanite City ili tuweze kushiriki kikamilifu kutengeneza fursa za kiuchumi
zitakauzo tufaidisha watanzania wote kwa maendeleo ya wote!
Thursday, October 12, 2017
Tanzanite City Chunya Full Council Briefing Part 2
Sehemu ya pili ya mkutano wa utambulisho wa Tanzanite City kwa wakuu wa idara na madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Chunya ambako ndiko jiji linajengwa.
Wednesday, October 11, 2017
KWA NINI TANZANITE CITY NI MUHIMU KWA MAPINDUNZI YA VIWANDA TANZANIA!!!
DHUMUNI KUU
Tanzanite City ni jiji la sayansi, teknolojia na ubunifu ambalo
lipo njiani kujengwa mkoani Mbeya katka wilaya ya Chunya. Jiji hili linajengwa kwa ushirikiano kati ya ESTA-TZ na ofisi ya mkuu wa mkoa, Mh. Amos Makalla, ofisi
ya Mkuu wa Wilaya ya Chunya, Mkurugenzi na Balaza la Madiwani wa Halmashauri ya
wilaya ya Chunya.
Lengo kuu la kuanzishwa kwa
Tanzanite City ni kujenga uwezo wa taifa letu kwenye mambo ya teknolojia na
kuhamasisha mapinduzi ya viwanda yatakayoifanya Tanzania kuwa kiwanda cha
Afrika na kitovu cha ubunifu katika ukanda huu wa Afrika kusini mwa jangwa la
Sahara.
Jiji hili litasaidia kuwajengea uwezo wa ubunifu katika maswala
teknolojia, vijana wanaomaliza vyuo katika fani za sayansi na teknolojia, na
kuwawezesha kuanzisha viwanda na kuunda makampuni watakayo yaendesha kwa ubia
na wanachi wengine, kupitia klabu ya marafiki wa Tanzanite City
BAADHI YA CHANGAMOTO TUNAZOKWENDA KUZIJIBU
Kama
tujuavyo serikali yaawamu ya tano ya Mh.
John Pombe Magufuli imedhamiria kuipeleka Tanzania kwenye uchumi wa viwanda,
Lakini katika safari hiyo kuna changamoto kadhaa ambazo ni lazima zifanyiwe kazi.
· Mazingira magumu na
yasiyo rafiki yanayoyoua utamaduni wa kuwekeza katika
viwanda yanawafanya watanzania wengi kuagiza bidhaa za viwanda toka nje,
· Kukosekana kwa
kiunganishi kati ya wanjasiriamali wazawa na wawekezaji wa nje kunakotokana na tofauti kubwa sana katika technoljia. Tofauti hii
imefanya kuwa vigumu sana kwa wazawa kuweza kuhamisha teknolojia toka ng’ambo
hivyo kudumaza kabisa uwezo wetu na kutufanya tuendelee kuwa tegemezi
· Kukosekana kwa
mikakati sahihi ya kukuza na kuendeleza teknolojia ambayo
imefanya Kushindwa kubadli mafanikio ya tafiti kuwa viwanda (industrialization
of applied research); kushindwa kugeuza viwanda kuwa fursa za kibishara ambako
ndiko pesa ilipo.
SULUHISHO LETU
Ili
kujibu changamoto hizo, jiji la Tanzanite City limeanzishiwa kwa lengo la
kuweka mazingira bora ya kukuzwa ubunifu na kuanzishwa kwa viwanda na
makampuni. MAMBO SITA MUHIMU YATAKAYOFANYWA
NA TANZANITE CITY
1. Miundombinu bora (infrastructures
and sound facilities)
2.
Mikakati mahususi ya kukuza
vipaji na ubunifu
3.
Upatikanaji wa mitaji na
fedha
4.
Upatikanaji wa huduma
mbalimbali
5.
Kujenga mfumo madhubuti wa
biashara (Adequate business systems);
6.
Kutangaza na kukuza taasisi
za wajasiliamali na ujasiliamali (Promotion of SMIEs and entrepreneurship);
JIJI LITAKAVYOFANYA KAZI
Watu
wenye vipaji toka kokote kule duniani wataalikwa kushirikiana na vijana wetu
wataalam katika fani za Sayansi na teknolojia wanaohitimu vyuo ambao watawekwa
kwenye makambi ya teknlojia (classified technology development camps), katika jiji hili ili waweze kubuni na kujenga
uwezo wa kutengeneza bidhaa mbalimbali za kitechnolojia huku wakipewa kila aina
ya msaada watakaohitaji, kuanzisha viwanda pamoja na kuanzisha makampuni
watakayoyamiliki kwa ushirika na watanzania wengine kupititia Klabu ya marafiki
wa Tanzanite City.
Vijana hawa wataalam
watapewa mission mahususi za kubuni na kujenga uweza wa kuzalisha teknlojia
kulingana na vipaumbele na mahitaji soko, kukopi teknolojia ambazo tayari zipo,
kuzifanyia maboresho kulingana na mahitaji ya soko, na kuanzisha bidhaa na
teknoljia mpya ambazo ni zetu wenyewe baada ya kuwa tumejenga uwezo wa kutosha.
Lengo ni kujenga
uwezo wetu wa ndani wa kuzalisha bidhaa za kiviwanda na kiteknoljia, kwa mfano
badala ya kuuza simu toka nchi za Asia, tuunda na kuuza simu zetu wenyewe!
Badala ya kuifuata Guangzhou kule Uchina tunataka kujenga Guangzhou yetu hapa
hapa nchini
TUNAHITAJI NINI TOKA KWAKO MDAU
Tunawataka
wanachi na wadau wengine kujiunga na
klabu ili;
Kwanza waweze
kuchangia kwenye ujenzi wa jiji kwa
fedha au mawazo
Pili waweze kushiriki
kikamilifu kwenye ujenzi wa Tanzania mpya
Wewe kama mdau muhimu
tunakuaomba tuungane na Mh Rais John Pombe Magufuli na mkuu wetu wa Mkoa ambaye
pamoja , Wabunge wetu katkia juhudi zao za kuleta maendeleo ya Viwanda na
kukuza uchumi wa Mkoa wetu .
TUMEDHARIA
KUIFANYA MBEYA KUWA GUANGZHOU YA AFRIKA,
Tanzanite City Chunya Full Council Briefing Part 1
Sehemu ya kwanza ya mkutano wa utambulisho wa Tanzanite City kwa wakuu wa idara na madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Chunya ambako ndiko jiji linajengwa.
Sunday, October 8, 2017
TANZANITE CITY YASHIRIKI VILIVYO KATIKA JUKWAA LA UWEKEZAJI MBEYA
Salaam za pongezi kwa Mh. Dr. Mary Mwanjelwa (Naibu Waziri Mteule wa Kilimo)
![]() |
Mheshimiwa Dr. Mary Mwanjelwa, Naibu Waziri Mteule Wa Kilimo |
Kamati
ya uongozi inayoshugulikia ujenzi wa jiji la sayansi, teknolojia na ubunifu la
Tanzanite City – Chunya, pamoja na wadau wetu wote kupitia klabu ya marafiki wa
Tanzanite City, tunapenda kutoa pongezi zetu za dhati kabisa kwa mbunge wetu wa
Mbeya na mdau wa Tanzanite City, Mheshimiwa Dr. MARY MWANJELWA kwa kuteuliwa
kwake na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. John Pombe Magufuli Kuwa
Naibu Waziri wa Kilimo.
Tunatambua
uwezo mkubwa sana alionao Mh. Mwanjelwa katika kutekeleza majukumu yake. Sisi kama
wadau wa maendeleo ya viwanda na Teknolojia tunatambua jukumu kubwa na zito
analokwenda kulibeba Mh Mwanjelwa, si mchezo-mchezo bali anatakiwa kuwa mbunifu
sana na asiyechoka kujifunza. Nchi yetu ni kubwa sana na ina matatizo mengi mno
yanayohusiana na wizara anayokwenda kuifanyia kazi.
Moja
ya changamoto ambazo Mh. Naibu Waziri atakutana nazo katika utekelezaji wa
majukumu yake ni matumizi duni ya teknolojia katika kilimo kwa ujumla wake na namna
ya kuongeza thamani ya mazao ya kilimo. Katika wakati huu ambao taifa letu lipo
kwenye kipindi cha mpito kuelekea uchumi wa kiviwanda, suala la teknolojia
linapaswa kupewa kipaumbele kwani linagusa kila Nyanja ya kilimo, kuanzia
kwenye maandalizi ya ardhi ikiwa ni pamoja na kuilima, kupanda na kupandikiza
mazao mashambani, kutunza mazao yaliyoshambani ili yaweze kutoa matunda bora na
ya kutosha, uvunaji wa mazao na kuyasafirisha toka mashambani, uhifadhi wa
mazao ghafi ya kilimo pamoja na kuyaongezea thamani. Yote hayo yanahitaji
teknolojia kwa mapana yake!
Mh.
Naibu Waziri, ni vigumu sana kuweza kuendelea kama taifa, iwe ni kwenye kilimo,
viwanda au hata biashara tu, iwapo tutapuuza matumizi ya teknolojia. Lakini pamoja
na kutilia maanani matumizi hayo ya teknolojia, bado hatutaweza kufikia malengo
yetu ya kiuchumi kama tutaendelea kuwa tegemezi kwa kiteknolojia toka nje. Kwani
hao tunaowategemea wao pia wanavyo viapaumbele vyao ambavyo siyo lazima
vifanane na vyetu. Hivyo sasa ni jukumu letu kama kweli tunataka kwenda kwenye
uchumi wa kati, wa viwanda na kilimo cha kibiashara na chenye tija, kuanza sasa
kujenga uwezo wetu wenyewe kwenye mambo ya technolojia ambao ndiyo mhimili wa
hivyo viwanda na hicho kilimo tunachokitaka.
Mh.
Naibu Waziri, sisi tumeanza na Tanzanite City, ni safari ngumu na ndefu, lakini
tumedhamiria kufika mwisho, tunaamini kuwa, kwa kuwekeza kwenye vipaji vya
vijana wetu, na kuwasaidia kutimiza ndoto zao, tutabadilisha mustakabari wa
taifa letu na kuboresha sana kilimo chetu, tukishirikiana sisi wanachi, wadau
wa maendeleo, pamoja na serikali tunaweza kuifanya Tanzania kuwa kiwanda cha
Afrika, na kitovu cha ubunifu katika maswala ya teknolojia.
Mh.
Naibu Waziri, tuna jua NIA UNAYO, SABABU UNAYO NA UWEZO UNAO! Tunakuahidi ushirikiano
wetu, tunakuombea afya njema, hekima, na heshima kwa watu unaowaongoza, wengi
wamepita na hawajaacha alama yoyote baada ya wao kuondoka, na wewe hutaishi
milele kwenye hiyo nafasi, lakini tunatamani kuona alama za kazi zako zikidumu
daima kwa vizazi vingi vijavyo!! TUNAJUA NA TUNAAMINI UNAWEZA!!! Tuna kutakia
kila lililo la heri, ufanikiwa katika majukumu yako hayo kwa taifa letu, MUNGU
Akubariki na akulinde siku zote za maisha yako. Amina.
Wednesday, August 2, 2017
Subscribe to:
Posts (Atom)