Search This Blog

TANZANITE CITY: The Africa's Factory & Innovation Powerhouse!

TANZANITE CITY: The Africa's Factory & Innovation Powerhouse!
We Will Turn Bushes Into Highly Industrialized City

Saturday, October 14, 2017

TANZANITE CITY; FURSA MPYA NA MBEYA MPYA, KUELEKEA TANZANIA YA VIWANDA

Mpango wa ujenzi wa jiji la sayansi, teknolojia na ubunifu katika wilaya ya  Chunya mkoani Mbeya unatoa fursa nyingine ya kiuchumi kwa watanzania na wakaazi wa mkoa wa Mbeya.  Katika wakati ambapo nchi yetu ipo kwenye kipindi cha mpito kuelekea uchumi wa kati na wa viwanda, mkoa wa Mbeya chini ya uongozi wa Mh. Amosi Makalla kwa kushirikiana kampuni ya ESTA-TZ na uongozi mzima wa wilaya na halmashauri ya wilaya ya Chunya umeanzisha mpango maalum wa kuifanya Mbeya kuwa kitovu cha maendeleo ya teknolojia na mapinduzi ya viwanda katika bara letu la Africa kusini mwa jangwa la sahara.
Katika mpango huu ambao eneo la kuanzia, kiasi cha kilomita za mraba miatano (500sqKm) katika wilaya ya Chunya, litatumika kujenga jiji la Tanzanite. Lengo kuu likiwa ni kuondoa utegemezi wa taifa letu kwa bidhaa na teknolojia mabalilmbali toka nje ya nchi. Katika kipindi cha miaka kumi na tano ijayo Tanzanite city inatarajiwa kujenga uwezo wa taifa letu katika ubunifu wa teknolojia na uzalishaji wa viwandani.
Ili kufikia lengo ambalo mkoa wa Mbeya umejiwekea kufikia mwaka 2030, mkakati mahsusi umewekwa wa kuwekeza kwa Vijana wenye vipaji wanaohitimu kutoka katika taasisi zetu za elimu ya juu.  Pindi wanapohitimu masomo yao, Vijana hao watakuwa wanawekwa kwenye makambi maalumu ya teknlolojia ndani ya jiji la Tanzanite, ambako huko watapewa kila kitu wanachohitaji kuweza kujenge uwezo katika masuala ya ubunifu wa teknolojia na uzalishaji. Vijana hawa watakuwa wanapatiwa mafunzo maalumu ya kuwawezesha kuanzisha na kuendeleza viwanda vitakavyotokana na kazi za kibunifu watakazokuwa wanazifanya makambini.
Mpango huu utawawezesha wazawa wote bila kujali mazingira wanayotoka au asili ya mtu, kuweza kumiliki viwanda kwa pamoja na vijana wabunifu ambao ndiyo watakuwa wakurugenzi wa makampuni hayo yatakayoundwa. Hadi sasa kuna maeneo zaidi ya mia tatu (300 Technology development missions) ambayo yapo tayari kuanza kufanyiwa kazi na vijana pindi ujenzi wa awali wa miundo mbinu muhimu utakapokamilika. Inatarajiwa kwamba maandalizi ya awali ya ujenzi wa Tanzanite City yatakamilika mwishoni mwa robo ya kwanza mwakani (March 2018) ambapo jiji litaanza rasmi shughuli zake.
Miezi sita baadaye viwanda visivyopungua 60 vitaanzishwa na kutoa ajira za moja kwa moja kiasi cha 1200. Baada ya hapo kila wiki kutakuwa na viwanda vipya vinaanzishwa na idadi yake itakuwa ikiongezeka siku hadi siku ambapo katika miaka 15 hadi 2030 jumla makmpuni  54,600 yanatarajiwa kuanzishwa na kutoa ajira za moja kwa moja zisozopungua milioni mbili na nusu.
Tafiti zinaonyesha kuwa kila ajira moja rasmi inazalisha ajira kati ya tatu hadi tano zisizokuwa rasmi. Hivyo katika kipindi cha miaka kumi na tano ijayo Tanzanite City itaweza kuzalisha ajira kwa watu wanaokaribia milioni saba. Sehemu kubwa ya watu hawa pamoja na familia zao watakuwa wanaishi ndani ya wilaya ya Chunya na maeneo jirani katika mikoa ya Songwe na Mbeya. Idadi hii ya watu itahitaji miundombinu mbalimbali ambayo Tanzanite City imejiandaa kikamilifu kuijenga kwa kushirikiana na marafiki pamoja na wadau wetu wote wa maendeleo katika mkoa wa Mbeya.
Tanzanite City inaleta fursa ya kipekee kwa wakazi wa Mbeya, na watanzania wote kwa ujumla, kwani kupitia klabu ya marafiki wa Tanzanite City kila mwanzanchi Mtanzania ataweza kushiriki kwa namna moja au nyingine katika kujenga uchumi wa viwanda. Lakini pia kupitia klabu ya marafiki wa Tanzanite City, watoto wa watanzania masikini wataweza kupata fursa ya kutumia vipaji vyao kubuni teknolojia na kuanzisha makampuni watakayoyamiliki kwa pamoja na watanzania wengine ambao pia ni wanachama wa klabu. Jambo hili lisingewezekana bila ya Tanzanite City. Kwa utaratibu huu hakuna mtanzania atakayeachwa nje ya uchumi wa viwanda kama atakuwa mwanachama wa klabu isipokuwa kwa mapenzi yake mwenyewe!
Klabu ya marafiki wa Tanzanite City ni chombo muhimu sana kwa ujenzi wa jiji la Tanzanite na uchumi wa viwanda kama tunavyotaka kwa sababu kuu mbilli; moja ni kuwa, klabu ndiyo njia pekee ya uhakika itakayowaunganisha watanzania wote na kuwapatia fursa ya kushiriki kikamilifu katika ujenzi wa Tanzania ya viwanda kama wadau na wamiliki. Pili, klabu kupitia michango na ada za wanachama ni chanzo muhimu cha mapato yatakayowezesha kugharimia shughuli na miradi mbalimbali ya ujenzi wa jiji na uendelezaji teknolojia. Wananchi kupitia klabu watafaidika na fursa nyingi sana zitakazotokana na ujenzi wa jiji hili hasa katika maeneo ya miundombinu, na huduma.
Kwa kuzingatia kuwa jiji la Tanzanite litakuwa kiwanda na kitovu cha mapinduzi ya viwanda na maendeleo ya teknlojia katika ukanda huu wa maziwa makuu ya Afrika, watu kutoka mataifa mbalimbali ya afrika watakuja Mbeya aidha kama watalii, wawekezaji ama wafanya biashara, hivyo kupelekea kuwa na fursa nyingi sana, baadhi nimeziorodhesha hapa:
1.         Huduma;
Usafiri na usafirishaji wa watu na mizigo, huduma za hoteli na mikahawa, huduma za afya, elimu ya msingi, secondary na vyuo (mahitaji ya vyuo ni makubwa kiasi cha kuhitajika vyuo zaidi 16 vitavyo toa kozi maalumu zinazoendana na mahitaji ya shughuli za Tanzanite City), ukusanyaji wa taka ngumu, huduma za ulinzi na usalama, huduma za simu na data, n.k.
2.         Miundombinu
Ujenzi wa barabara, mitandao ya maji safi na maji taka, uzalishaji na usambazaji wa umeme, mawasiliano, n.k.
3.         Ujenzi wa nyumba
Nyumba za kuishi, majengo ya biashara, ofisi na viwanda
4.         Biashara
Bima, mabenki, maduka makubwa (Malls), wasambazaji wa bidhaa zinazozalishwa ndani ya jiji, wauzaji wa bidhaa kwa matumizi ya nyumbani kama vyakula na vifaa vingine, sehemu za burudani, n.k.
Ili mtu aweze kunufaika na fursa hizo, ni sharti awe mwanachama wa klabu ya marafiki wa Tanzanite City, kwa maana nyingine anatakiwa kuwa RAFIKI wa Tanzanite City. Rafiki wa kweli ni mtu ambaye yupo tayari kujitoa kwa kila hali kwa ajili ya manufaa ya rafiki yake hata kama yeye mwenyewe hafaidiki moja kwa moja na kujitoa huko. Marafiki wa Tanzaite City watakuwa tayari kuichangia Tanzanite City kwa kulipia ada zao za uwanachama kwa wakati ili kuwawezesha vijana wa watanzania kutimiza ndoto zao na kuigeuza dunia kuwa wanachotaka. Kupitia klabu hii siyo lazima kuwa kila utakachochangia lazima kikunufaishe, mchango wako utakuwezesha kuwa miongoni mwa wadau watakoweza kunufaika na fursa ambazo michango yanu kama marafiki itakuwa imetumika kuzitengeneza kupita vijana wetu wenye vipaji watakaokuwa makambini.
Ni wazi kuwa sasa wanachi wa mkoa wa Mbeya na watanzania wangine wote tunapaswa kumuunga mkono mkuu wa mkoa Mh. Amosi Makalla, mkuu wa wilaya na uongozi mzima wa halmashauri ya wilaya ya Chunya, kwa kujiunga na klabu ya marafiki wa Tanzanite City ili tuweze kushiriki kikamilifu kutengeneza fursa za kiuchumi zitakauzo tufaidisha watanzania wote kwa maendeleo ya wote!  


No comments:

Post a Comment