Search This Blog

TANZANITE CITY: The Africa's Factory & Innovation Powerhouse!

TANZANITE CITY: The Africa's Factory & Innovation Powerhouse!
We Will Turn Bushes Into Highly Industrialized City

Wednesday, November 20, 2013

Tunahimiza mapinduzi ya teknolojia katikati ya nguvu za giza!


Bundi: Alama/Ishara ya ushirina na uchawi
Mabadiliko katika tasnia ya sayansi na teknolojia, uchumi wa kisasa na mfumo wa utandawazi na soko huria, umelata mabadiliko makubwa sana katika mfumo wa maisha ya watu wengi katika mataifa mengi duniani husasi nchi masikini za dunia ya tatu kama Tanzania ambazo uchumi wake unategemea sana uchumi wa  nje.
Mapinduzi ya kiteknolojia yanatokana na kazi za utafiti wa kiasayansi na siyo matunguli
Kwa ujumla kuna watu wengi ambao wameneemeka na mabadiliko hayo ya uchumi kwani yameletea fursa nyingi za kiuchumi  ambazo hapo mwanzo hawakuwa nazo kutokana na mfumo wa biashara uliokuwapo hasa wakati wa vita baridi iliyomazika mwishoni mwa miaka ya themanini.  Watu waliopokea mabadiiko hayo kwa mtazamo chanya zaidi wameweza kujilimbikizia fedha na mali nyingi katika kipindi kifupi sana ukilinganisha na wakati mwingine wowote ule ambao dunia imekuwa ikipitia katika misuko suko ya kiuchumi kama hii ya sasa. Biashara nyingi zimenzishwa, teknolojia mpya zinagunduliwa kila uchao na mamilioni ya watu wanafurahia na kufaidi matunda ya uhuru wa habari na mawasiliano, uhuru ambao hautambui mipaka ya kijiografia wala ya kiitikadi. Hivi sasa watu waliopo katika maeneo tofauti kijiografia wanaweza kuendesha na kufanya vikao, mikutano, makongamano, semina na hata majadiliano ya kibiashara bila ya kujali umbali baina yao utadhani wote wapo katika chumba kimoja. Heko teknolojia ya habari na mawasiano.
Wakati wanasayansi wenzetu wanaota kuishi nje ya sayari ya dunia,
 sisi tunamikakati gani ya kuelekea huko?
Katika nchi yetu matunda ya maendeleo yaliyotokana na mabadiliko ya hayo hayajaweza kuwafikia na kuwafaidisha watu wengi sana kama ambavyo ilitarajiwa. Zaidi ya kuwa mabadiliko hayo yamenaonekana kuwanufaisha zaidi watu wachache katika nchi yetu ambao wengi wao ni wafanyabiashara, wanasiasa katika ngazi za juu za utawala na maamuzi na wasomi wa daraja wa daraja la kati wanaojipatia kipato kikubwa kutokana na fursa walizonazo katika ajira zao. Masikini na watu wenye kipato cha kawaida wameachwa pembezoni wakiwa watazamaji bila ya matumaini wala matarajio yoyote. Jambo hili limepelea kuzidi kuongezeka kwa pengo kati ya walionacho na wasionacho kwa kiasi ambacho kama hatua za makusudi hazitachukuliwa basi muda si mwingi ujao huwenda inchi yetu ikawa si mahali salama sana per kuishi kama tulivyozowea.
Wakati wachawi wakitumia unga, fagio na pembe na vitu vingine visivyoonekana kusafiria, wanasayansi wana fanya kazi kubwa kugundua na kuunda mashuine halisi zinazoleta mapinduzi ya kweli kwa mmaisha ya watu
Wakati ambapo baadhi ya watu waliofanikiwa kwa kiasi kikubwa katika maisha wakionekana kama mfano wa kuigwa katika jamii yetu kuna jamba moja ambalo kwa kweli linatia hofu japo kwa sasa inaonekana kama sehemu muhimu sana katika maisha. Sio ajabu hapa nchini kusikia kuwa baadhi ya watu maarufu wakiwemo wanasiasa, wafanyabiashara na wafanyakazi bila kujali kiwango cha ufahamu au elimu zao kuwa mafanikio waliyonayo yanachangiwa kwa kiasi kikubwa na nguvu za giza! Tumeshazowea kushuhudia wanasiasa wakipishana bila idadi kwa sangoma kule mlingotini wakisaka ubunge au madaraka mengine ya kisiasa! Inashangaza sana kwamba viongozi wetu hawaamini kama watu waliowachagua walifanya hivyo hivyo kwa kuwaamini matokeo yake wanatafuta mbinu za kichawi ili kuwaroga wapigakura wao au mabosi wa ili wawachague na kuwapa ulaji wanaoutaka. Tunajua viongozi wengi ambao wanapata madaraka kwa njia za kichawi, mara nyingi hawajiamini kwenye manbo ya kimsingi lakini majibu yao yamejaa kiburi, jeuri na kejeli, wanajua watu waliowapa madaraka walionayo hawana uwezo wa kuwaondoa kwani hata hivyo hawakuwapa kwa dhamira zao binafsi bali kwa nguvu za giza
Wafanyabiashara kwa upande wao nao kila kukicha wanashindana kwa waganga kutafuta madawa ya kuvuta utajiri zaidi na kung’arisha nyota zao, wao wapo tayari hata kutoa uhai wa binadamu wenzao ilimradi tu wapete mali zaidi, huu ni ubinafsi uliovuka mipaka kiasi ambacho huwezi kuelezea, wengine wamedirika hata kufanya ngono na wazazi wao ili wapate hiyo mali na utajiri wanaousaka usiku na mchana. Hali haiko tofauti huko maofisini, ambako wafanyakazia katika kada mbalimbali nao wanakesha kwa wataalam kutafuta bahati ya kupandinshwa cheo, kulinda kazi zao zisiwaponyoke, au kuongezwa mishahara na kupewa upendeleo katika mambo mbalimbali ya kikazi. Kwa maaskofu na mashehe huko hali ndiyo mbaya zaidi, sasa siyo ushirikina peke yake, wapo baadhi wanauza hata madawa ya kulevya kupitia makanisa yao!


Mganga wa kienyeji mitaani Afrika Kusini
Hali inatisha zaidi pale serikali inaposhadadia nguvu zisizoonekana kwa kisingizio cha kuiombea nchi, wanasiasa hawajiulizi mara mbili kuwakusanya wananchi kwa maelfu kufanya maombi pale taifa linapokabiliwa na tishio fulani iwe la kisiasa, kiuchumi au kijamii. Kwenye michezo hili ndiyo imekuwa ada, bila maombi timu zetu hakuna kitu, utamsikia kiongozi wa soka akiwahimiza wananchi “ndugu wananchi tuiombee timu yetu ya taifa katika mchezo wa leo iweze kushinda kwani mchezo huu ni wa muhimu sana…” utadhani wapinzani wetu wao hawamjui Mungu au tunategemea mwenyezi Mungu amtume roho mtakatifu kama alivyofanya kwa wale mitume 11 wa bwana Yesu ili waweze kucheza na kupata ushindi. Naomba hapa ieleweke kwamba sipingi kumuomba mwenyezi Mungu kwa lolote lile, tatizo langu liko kwetu sisi wenyewe, kuwa tumefanya nini kilichondani ya uwezo wetu kuweza kufanya vizuri kabla hatujamgeukia Mwenyezi Mungu? Au ndiyo tunategemea muujiza kama ule wa babu wa Loliondo?  Hii inatisha sana hasa kwa taifa changa kama letu ambalo tunahitaji kukimbia kisayansi na kiteknoljia wakati wenzetu wanatembea ili tuweza kuondoa pengo la kimaendeleo baina yetu na mataifa mengine.
Pengine hatuwezi kushangaa sana kuwa hata serikali inashabikia imani za giza, kwa kuwa baadhi ya hao viongozi wanaoongoza hiyo serikali yenyewe pia wanaamini kuwa madaraka yao yametokana na msaada wa kichawi au nguvu za giza. Tunategemea nini kipya toka kwa viongozi kama hao? Tutakuwa wehu kama tutafikiri kuwa watu wanaweza kubadilika na kusaliti miungu wao, kamwe hawawezi kukemea mambo hayo pamoja na ukweli kuwa wanaelewa vema madhara yake kwa taifa letu na vizazi vyake.
Wengi huamini kuwa wachawi wanauwezo wa kufanya mambo ya ajabu 
ambayo hayawezekani kisayansi ikiwemo kusafiri kwa kutumia fagio, ungo, pembe n.k 
bila kujali elimu wala kanuni zinazotawala mwenendo wa dunia
Lakini labda mtu anaweza kujiuliza kuwa “ni kwa nini tunapinga imani hizi za kishirikina wakati kuna watu wengi wameweza kupata mafanikio makubwa sana na kutoa mchango mkubwa katika maendeleo ya taifa?”
Kwanza kabisa ni lazima tuelewe kuwa ushirikina ni ishara ya wazi ya mtu aliyeshiwa mbinu na mikakati ya kimaisha, ni alama ya mtu ambaye hana jipya katika fikra zake na amefika mahali haoni suluhu yoyote ya matatizo yanayomkabili iwe ya kiuchumi, kijamii, kisiasa au hata mahitaji ya binfsi ya kibinadamu. Mtu anapofikia hatua hiyo hukabliwa na msongo wa mawazo na ni rahisi sana kushawishika kuingia kufanya jambo lolote lile litakaloelekea kumpatia ahue ya muda bila kujali athari za baadaye za matendo yake.
Wataalamu wakifanyia majaribio "Memory" ya simu ya mkononi, 
ushirikina hauwezi kwenda sambamba na kazi za kisayansi!
Tatizo kubwa la imani hizi za kishirikina ni kuwa zinadhoofisha na kudumaza kabisa uwezo wa watu wa kufikiria (Brainstorming Power). Wanashindwa kuona nguvu na uwezo uliyomo ndani yao, wanaweka kando elimu zao na hawaamini tena vipaji vyao, matokeo yake wanakuwa watumwa wa matapeli wanaojiita wataalam  ambao wameena na mabango yao kila kona za miji yetu wakichuma bila jasho mali za wajinga (wajinga ndiyo waliwao). Matapeli hawa wamekuwa wajanja sana na wanatumia mbinu za hali ya juu utaalamu wa masoko na saikolojiainu zao kwa kufuata maitaji ya wakati husikana ni wepesi sana kusoma hisia za wateja wao na wanajua sana namna ya kushughulika na hisia zao.
Jambo moja kubwa ambalo tunaweza kujifunza kutokana na biashara hii ya nguvu za giza na ambalo linaweza kuwa na manufaa makubwa jamii yetu ni namna watu hawa wanavyoweza kucheza na akili wa watu na kufanya kila kitu kionekane kuwa halisia, hisia hizo huwafanya watu hao kuwa na imani kubwa kiasi ambacho hawaamini kabisa kwamba kuna kushindwa katika maisha wakiwa na nguvu za giza. Nguvu hizo huwa kubwa kiasi cha kumfanya muhusika kufanya jambo lolote katika maisha bila kujali kupata athari mbaya, watu hawa huvaa ushujaa ambao unawafanya wasiweze kushindwa kitu. Lakini kutokana na ukweli kuwa watu wetu hawana elimu ya jinsi akili na ubongo wa binadamu unavyofanya kazi wanadhani ni damu za mbuzi au viungo vya albino vinavyowaletea mafanikio, jambo ambalo yawezekana likawa na ukweli japo ni kweli pia kuwa waganga wengi ni matapeli na dawa zao hazina owezo huo.
Uchawi pia unahusishwa na nguvu na uwezo wa ajabu unaopita uhalisia wa kibinadamu
Zama hizi ambazo sayansi na teknolojia vinatawala kila kitu watanzania tuna kazi ya ziada kuwaelimisha wanachi wetu juu ya kanuni za zinazotawala mfumo wa fahamu wa mwanadamu na mawasiliano ya nafsi. Kanuni hizo ni muhimu sana kwa mafanikio ya mtu mmoja mmoja na jamii nzima kwa jumla. Hivi sasa msisitizo mkubwa kwa wanachi na wasomi katika jamii zetu ni kujiajiri katika sekta binafsi jambo ambalo kama hatuna maandalizi mazuri kwa watu wetu tutaishia kwa wachawi na matapeli. Tunapashwa kama taifa kuwaandaa watu wetu kisaikolojia na elimu inayotawala kanuni za mafanikio, matumizi sahihi ya fedha, uewekezaji, masoko n.k. elimu hii haitolewi katika vyuo wala mashule yetu na watu wanaotoka katika vyuo hivyo huwa hawajui chochote kabisa kitu kinachowaingiza kwenye matumizi ya anasa nayasiyokuwa na maana matokea yake wanishia kukimbilia kwa masangoma.
Watu ambao tumekuwa tukidhani kuwa ni wasomi na wataalamu wa mambo mbali mbali katika jamii na ambao tunawamini kutushauri kila siku kwenye biashara zetu n.k. utkakuta kuwa wao wenyewe hawana kitu na hata hizo biashara wanazoshauri wao hawazifanyi – utakutana na mtaalamu elekezi wa biashara anashauri juu uendeshaji wa maduka lakini yeye menyewe hata genge linamshinda kusimamia. Tunayaona haya kwenye mikataba mbalimbali ambayo wataalam wetu wanaiingizwa mkenge aidha kwa makusudi au kwa kutojua.  Wanahubiri yale wasioyatenda, ambavyo wao wenyewe hawayaamini lakini mwisho wa siku lawama zote wanatupiwa wananchi masikini kwa ujinga wao.
Safari ni ndefu lakini lazima tuianze sasa! Hatuna muda zaidi wa kusubiri vinginevyo tuwe tayari kujisalimisha kwa wakoloni kwa mara nyingine watutawale na kutupa mkate wa siku huku tukiwa makolokoloni na mayaya majumbani kwao na wao akifanyakazi kwenye miradi ya kuhamisha rasilimali za taifa letu.


No comments:

Post a Comment