Search This Blog

TANZANITE CITY: The Africa's Factory & Innovation Powerhouse!

TANZANITE CITY: The Africa's Factory & Innovation Powerhouse!
We Will Turn Bushes Into Highly Industrialized City

Sunday, February 4, 2018

Tanzanite City Inasonga Mbele!

Vijana wataalamu katika fani mbalimbali toka katika vyuo vyetu vikuu wakiwa katka sehemu ya mijadala kuhusiana na maendeleo ya ujenzi wa jiji la sayansi, teknolojia na ubunifu; Tanzanite  City.

Sunday, October 22, 2017

Tanzanite City Part 02: Tuliyojifunza Toka Kwa Wengine!

Wazo la kuanzishwa kwa Tanzanite City limetokana na tafiti nyingi tulizozifanya kwa kipindi cha zaidi ya miaka kumi iliyopita. Tafiti hizo zililenga kutufanya tujue wenzetu waliokuwa na ndoto kama zetu walipitia changamoto zipi, na kama waliweza kufaulu walifanya nini cha tofauti na kama walifeli walikosea wapi. Vilevile tulilenga kutambua mifumo na mikakati sahihi ya kufuata ili kuweza kuwa na mafanikio tunayohitaji kuifikia Tanzania ya viwanda. Mambo yafuatayo tuliyazingatia kwenye tafiti zetu:
a.     Tuliangalia matarajio na mwenendo wa masuala ya teknolojia na ubunifu pamoja na mabadiliko katika uchumi wa dunia
b.     Historia na uzoefu wetu hapa nyumbani na wa mataifa mengine katika masuala ya sayansi na teknolojia pamoja na maendeleo ya kitaasisi.
c.     Tuliangalia hali halisi ya sasa, uwezo na rasilimali tulizonazo, miundo ya kitaasisi na mikakati yetu kama taifa
d.     Tukafanya upembuzi wa mafanikio na matatizo/changamoto ambazo mataifa mengine yaliyokuwa na malengo kama yetu walipitia katika kufikia malengo yao.
Tafiti hizo zilituonyesha kuwa, iwapo tutatengeneza mazingira hamasishi kwa shughuli za utafiti na ubunifu pamoja na kuwezesha uanzishaji wa makampuni kwa utaratibu rahisi na rafiki kisha kuwavutia wawekezaji wa nje kuingia ubia na watanzania, Tanzania inaweza kabisa kupiga hatua kubwa katika mapinduzi ya teknolojia na viwanda sawa kabisa na mataifa mengine yote yaliyoendelea ikiwamo Uchina, india, Indonesia, Malaysia n.k.
Kwa hiyo mchakato wa ujenzi wa Tanzanite city unatokana na uzoefu tulioupata kutoka kwa mataifa ambayo yamefanikiwa kupata maendeleo makubwa ya kiteknolojia na kiviwanda katika miongo michache iliyopita. Swala la msingi ni kuhakikisha kuwa mchakato mzima unaendana na hali halisi na changamoto mahsusi za taifa letu na mazingira yaliyopo. Vile vile, mchakato mzima lazima ujikite katika mipango halisi na inayotekelezeka.
Ili kuweza kukidhi mahitaji ya kuipeleka Tanzania kwenye uchumi wa viwanda, uanzishwaji wa jiji la Tanzanite City umezingatia mambo yafuatayo ambayo ni ya msingi:
a.    Mkakati mahususi (Focused strategy); mkakati mahsusi wa ujenzi wa Tanzanite City ni kujenga na kuimarisha uwezo wetu wa ndani wa kubuni teknolojia na kuanzisha viwanda pamoja na makampuni ya teknolojia. Kuwashirikisha watanzania wazawa kupitia klabu ya marafiki wa Tanzanite City kumiliki viwanda na makampuni badala ya kubaki watazamaji tu ndani ya nchi yao.
b.    Miundombinu inayokidhi haja maridhawa (Sound facilities & infrastructures); ujenzi wa miundombinu muhimu utawanufaisha wanasayansi na wabunifu wetu kwa kuwawezesha kufanya tafiti zao kwa uhakika na kujiamini.
c.     Kujenga mfumo madhubuti wa biashara (Adequate business systems); mfumo madhubuti wa kibiashara utarahisisha upatikanaji wa huduma muhimu na kuvutia wawekezaji, wafanyabiashara na wajasilamali pamoja na wataalam mbalimbali katika fani zote kuja kuwekeza rasilimali zao Tanzanite City.
d.    Ukuzaji wa teknolojia na vipaji (Development of talents and technology); kukuza vipaji na uendelezaji wa teknolojia kwa kuwajengea uwezo vijana wanaomaliza katika taasisi zetu za elimu ya juu na kuwawezesha kubuni teknolojia na vifaa vya uzalishaji pamoja na kuwasaidia kujenga viwanda na kuanzisha makampuni.
e.    Kuwezesha upatikanaji wa mitaji na fedha (Access to capital and financing); moja ya matatizo makubwa ya wajasiliamali na wataalam wa teknolojia hapa nchini ni upatikanaji mgumu wa mitaji na fedha za kugharimia tafiti na kubunifu. Tanzanite City ina mkakati wa makusudi wa kuhakikisha kuna upatikanaji wa uhakika wa fedha za mitaji na kuendeshea tafiti mbalimbali. Lengo ni kuwafanya wataalam wetu wazingatie zaidi shughuli za kitafiti badala ya kufikiria namna ya kupata pesa kwa ajili ya kuendesha maisha pamoja na kujikimu wao wenyewe.
f.      Kusaidia kupromoti taasisi za wajasiliamali na ujasiliamali (Promotion of SMIEs and entrepreneurship); baada ya wataalam wetu kubuni teknlolojia na bidhaa zao kwa ufanisi, kujenga uwezo wa kuzalisha kwa wingi na kwa viwango vya kimataifa, kitakachofuata ni kuwasaidia kujenga viwanda na kuanzisha makampuni watakayo yamiliki kwa ubia na watanzania wengine kupitia klabu ya marafiki wa Tanzanite City. Makampuni haya ndiyo yatakayo tengeneza fursa za kibiashara ambazo ndizo zitakazowaletea fedha pamoja na kujenga  mahusiano baina ya watanzania na wawekezaji wa kigeni katika masuala ya teknlolojia na viwanda
MTANZANIA MWENZANGU UKIONA JAMBO HALIJAFANYIKA, JUA NI MIMI NA WEWE HATUJALIFANYA. ACHA LAWAMA NA UCHUKUE HATUA; JIUNGE NA KLABU YA MARAFIKI WA TANZANITE CITY USHIRIKI KUIJENGA TANZANIA MPYA YA VIWANDA KUPITIA TANZANITE CITY!
Kwa maelezo zaidi tembelea - https://esta-tanzanitecity.blogspot.com/p/friends-club-of-tanzanite-city.html
Katika sehemu itakayofuata (Tanzanite City - Part 03) tutazungumzia Klabu ya Marafiki wa Tanzanite City; nini lengo la kuanzishwa kwake, kwa nini ni muhimu ujiunge na klabu, fursa na faida za kuwa mwanachama au rafiki wa Tanzanite city n.k.  TWENDE PAMOJA HADI KIELEWEKE!

Tuesday, October 17, 2017

Tanzanite City Chunya Full Council Briefing Part 5



Sehemu ya tano ya mkutano wa utambulisho wa Tanzanite City kwa wakuu wa idara na madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Chunya ambako ndiko jiji linajengwa.

Tanzanite City Chunya Full Council Briefing Part 5



Sehemu ya tano ya mkutano wa utambulisho wa Tanzanite City kwa wakuu wa idara na madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Chunya ambako ndiko jiji linajengwa.

Tanzanite City Chunya Full Council Briefing Part 4



Sehemu ya nne ya mkutano wa utambulisho wa Tanzanite City kwa wakuu wa idara na madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Chunya ambako ndiko jiji linajengwa.

Sunday, October 15, 2017

Tanzanite City Chunya Full Council Briefing Part 3



Sehemu ya tatu ya mkutano wa utambulisho wa Tanzanite City kwa wakuu wa idara na madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Chunya ambako ndiko jiji linajengwa.

Saturday, October 14, 2017

TANZANITE CITY; FURSA MPYA NA MBEYA MPYA, KUELEKEA TANZANIA YA VIWANDA

Mpango wa ujenzi wa jiji la sayansi, teknolojia na ubunifu katika wilaya ya  Chunya mkoani Mbeya unatoa fursa nyingine ya kiuchumi kwa watanzania na wakaazi wa mkoa wa Mbeya.  Katika wakati ambapo nchi yetu ipo kwenye kipindi cha mpito kuelekea uchumi wa kati na wa viwanda, mkoa wa Mbeya chini ya uongozi wa Mh. Amosi Makalla kwa kushirikiana kampuni ya ESTA-TZ na uongozi mzima wa wilaya na halmashauri ya wilaya ya Chunya umeanzisha mpango maalum wa kuifanya Mbeya kuwa kitovu cha maendeleo ya teknolojia na mapinduzi ya viwanda katika bara letu la Africa kusini mwa jangwa la sahara.
Katika mpango huu ambao eneo la kuanzia, kiasi cha kilomita za mraba miatano (500sqKm) katika wilaya ya Chunya, litatumika kujenga jiji la Tanzanite. Lengo kuu likiwa ni kuondoa utegemezi wa taifa letu kwa bidhaa na teknolojia mabalilmbali toka nje ya nchi. Katika kipindi cha miaka kumi na tano ijayo Tanzanite city inatarajiwa kujenga uwezo wa taifa letu katika ubunifu wa teknolojia na uzalishaji wa viwandani.
Ili kufikia lengo ambalo mkoa wa Mbeya umejiwekea kufikia mwaka 2030, mkakati mahsusi umewekwa wa kuwekeza kwa Vijana wenye vipaji wanaohitimu kutoka katika taasisi zetu za elimu ya juu.  Pindi wanapohitimu masomo yao, Vijana hao watakuwa wanawekwa kwenye makambi maalumu ya teknlolojia ndani ya jiji la Tanzanite, ambako huko watapewa kila kitu wanachohitaji kuweza kujenge uwezo katika masuala ya ubunifu wa teknolojia na uzalishaji. Vijana hawa watakuwa wanapatiwa mafunzo maalumu ya kuwawezesha kuanzisha na kuendeleza viwanda vitakavyotokana na kazi za kibunifu watakazokuwa wanazifanya makambini.
Mpango huu utawawezesha wazawa wote bila kujali mazingira wanayotoka au asili ya mtu, kuweza kumiliki viwanda kwa pamoja na vijana wabunifu ambao ndiyo watakuwa wakurugenzi wa makampuni hayo yatakayoundwa. Hadi sasa kuna maeneo zaidi ya mia tatu (300 Technology development missions) ambayo yapo tayari kuanza kufanyiwa kazi na vijana pindi ujenzi wa awali wa miundo mbinu muhimu utakapokamilika. Inatarajiwa kwamba maandalizi ya awali ya ujenzi wa Tanzanite City yatakamilika mwishoni mwa robo ya kwanza mwakani (March 2018) ambapo jiji litaanza rasmi shughuli zake.
Miezi sita baadaye viwanda visivyopungua 60 vitaanzishwa na kutoa ajira za moja kwa moja kiasi cha 1200. Baada ya hapo kila wiki kutakuwa na viwanda vipya vinaanzishwa na idadi yake itakuwa ikiongezeka siku hadi siku ambapo katika miaka 15 hadi 2030 jumla makmpuni  54,600 yanatarajiwa kuanzishwa na kutoa ajira za moja kwa moja zisozopungua milioni mbili na nusu.
Tafiti zinaonyesha kuwa kila ajira moja rasmi inazalisha ajira kati ya tatu hadi tano zisizokuwa rasmi. Hivyo katika kipindi cha miaka kumi na tano ijayo Tanzanite City itaweza kuzalisha ajira kwa watu wanaokaribia milioni saba. Sehemu kubwa ya watu hawa pamoja na familia zao watakuwa wanaishi ndani ya wilaya ya Chunya na maeneo jirani katika mikoa ya Songwe na Mbeya. Idadi hii ya watu itahitaji miundombinu mbalimbali ambayo Tanzanite City imejiandaa kikamilifu kuijenga kwa kushirikiana na marafiki pamoja na wadau wetu wote wa maendeleo katika mkoa wa Mbeya.
Tanzanite City inaleta fursa ya kipekee kwa wakazi wa Mbeya, na watanzania wote kwa ujumla, kwani kupitia klabu ya marafiki wa Tanzanite City kila mwanzanchi Mtanzania ataweza kushiriki kwa namna moja au nyingine katika kujenga uchumi wa viwanda. Lakini pia kupitia klabu ya marafiki wa Tanzanite City, watoto wa watanzania masikini wataweza kupata fursa ya kutumia vipaji vyao kubuni teknolojia na kuanzisha makampuni watakayoyamiliki kwa pamoja na watanzania wengine ambao pia ni wanachama wa klabu. Jambo hili lisingewezekana bila ya Tanzanite City. Kwa utaratibu huu hakuna mtanzania atakayeachwa nje ya uchumi wa viwanda kama atakuwa mwanachama wa klabu isipokuwa kwa mapenzi yake mwenyewe!
Klabu ya marafiki wa Tanzanite City ni chombo muhimu sana kwa ujenzi wa jiji la Tanzanite na uchumi wa viwanda kama tunavyotaka kwa sababu kuu mbilli; moja ni kuwa, klabu ndiyo njia pekee ya uhakika itakayowaunganisha watanzania wote na kuwapatia fursa ya kushiriki kikamilifu katika ujenzi wa Tanzania ya viwanda kama wadau na wamiliki. Pili, klabu kupitia michango na ada za wanachama ni chanzo muhimu cha mapato yatakayowezesha kugharimia shughuli na miradi mbalimbali ya ujenzi wa jiji na uendelezaji teknolojia. Wananchi kupitia klabu watafaidika na fursa nyingi sana zitakazotokana na ujenzi wa jiji hili hasa katika maeneo ya miundombinu, na huduma.
Kwa kuzingatia kuwa jiji la Tanzanite litakuwa kiwanda na kitovu cha mapinduzi ya viwanda na maendeleo ya teknlojia katika ukanda huu wa maziwa makuu ya Afrika, watu kutoka mataifa mbalimbali ya afrika watakuja Mbeya aidha kama watalii, wawekezaji ama wafanya biashara, hivyo kupelekea kuwa na fursa nyingi sana, baadhi nimeziorodhesha hapa:
1.         Huduma;
Usafiri na usafirishaji wa watu na mizigo, huduma za hoteli na mikahawa, huduma za afya, elimu ya msingi, secondary na vyuo (mahitaji ya vyuo ni makubwa kiasi cha kuhitajika vyuo zaidi 16 vitavyo toa kozi maalumu zinazoendana na mahitaji ya shughuli za Tanzanite City), ukusanyaji wa taka ngumu, huduma za ulinzi na usalama, huduma za simu na data, n.k.
2.         Miundombinu
Ujenzi wa barabara, mitandao ya maji safi na maji taka, uzalishaji na usambazaji wa umeme, mawasiliano, n.k.
3.         Ujenzi wa nyumba
Nyumba za kuishi, majengo ya biashara, ofisi na viwanda
4.         Biashara
Bima, mabenki, maduka makubwa (Malls), wasambazaji wa bidhaa zinazozalishwa ndani ya jiji, wauzaji wa bidhaa kwa matumizi ya nyumbani kama vyakula na vifaa vingine, sehemu za burudani, n.k.
Ili mtu aweze kunufaika na fursa hizo, ni sharti awe mwanachama wa klabu ya marafiki wa Tanzanite City, kwa maana nyingine anatakiwa kuwa RAFIKI wa Tanzanite City. Rafiki wa kweli ni mtu ambaye yupo tayari kujitoa kwa kila hali kwa ajili ya manufaa ya rafiki yake hata kama yeye mwenyewe hafaidiki moja kwa moja na kujitoa huko. Marafiki wa Tanzaite City watakuwa tayari kuichangia Tanzanite City kwa kulipia ada zao za uwanachama kwa wakati ili kuwawezesha vijana wa watanzania kutimiza ndoto zao na kuigeuza dunia kuwa wanachotaka. Kupitia klabu hii siyo lazima kuwa kila utakachochangia lazima kikunufaishe, mchango wako utakuwezesha kuwa miongoni mwa wadau watakoweza kunufaika na fursa ambazo michango yanu kama marafiki itakuwa imetumika kuzitengeneza kupita vijana wetu wenye vipaji watakaokuwa makambini.
Ni wazi kuwa sasa wanachi wa mkoa wa Mbeya na watanzania wangine wote tunapaswa kumuunga mkono mkuu wa mkoa Mh. Amosi Makalla, mkuu wa wilaya na uongozi mzima wa halmashauri ya wilaya ya Chunya, kwa kujiunga na klabu ya marafiki wa Tanzanite City ili tuweze kushiriki kikamilifu kutengeneza fursa za kiuchumi zitakauzo tufaidisha watanzania wote kwa maendeleo ya wote!  


Thursday, October 12, 2017

Tanzanite City Chunya Full Council Briefing Part 2



Sehemu ya pili ya mkutano wa utambulisho wa Tanzanite City kwa wakuu wa idara na madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Chunya ambako ndiko jiji linajengwa.

Wednesday, October 11, 2017

KWA NINI TANZANITE CITY NI MUHIMU KWA MAPINDUNZI YA VIWANDA TANZANIA!!!

DHUMUNI KUU
Tanzanite City ni jiji la sayansi, teknolojia na ubunifu ambalo lipo njiani kujengwa mkoani Mbeya katka wilaya ya Chunya. Jiji hili linajengwa kwa ushirikiano kati ya ESTA-TZ na ofisi ya mkuu wa mkoa, Mh. Amos Makalla, ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Chunya, Mkurugenzi na Balaza la Madiwani wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya.
Lengo kuu la kuanzishwa kwa Tanzanite City ni kujenga uwezo wa taifa letu kwenye mambo ya teknolojia na kuhamasisha mapinduzi ya viwanda yatakayoifanya Tanzania kuwa kiwanda cha Afrika na kitovu cha ubunifu katika ukanda huu wa Afrika kusini mwa jangwa la Sahara.
Jiji hili litasaidia kuwajengea uwezo wa ubunifu katika maswala teknolojia, vijana wanaomaliza vyuo katika fani za sayansi na teknolojia, na kuwawezesha kuanzisha viwanda na kuunda makampuni watakayo yaendesha kwa ubia na wanachi wengine, kupitia klabu ya marafiki wa Tanzanite City
BAADHI YA CHANGAMOTO TUNAZOKWENDA KUZIJIBU
Kama tujuavyo serikali yaawamu ya tano ya  Mh. John Pombe Magufuli imedhamiria kuipeleka Tanzania kwenye uchumi wa viwanda, Lakini katika safari hiyo kuna changamoto kadhaa ambazo ni lazima  zifanyiwe kazi.
·       Mazingira magumu na yasiyo rafiki yanayoyoua utamaduni wa kuwekeza katika viwanda yanawafanya watanzania wengi kuagiza bidhaa za viwanda toka nje,
·       Kukosekana kwa kiunganishi kati ya wanjasiriamali wazawa na wawekezaji wa nje kunakotokana na tofauti kubwa sana katika technoljia. Tofauti hii imefanya kuwa vigumu sana kwa wazawa kuweza kuhamisha teknolojia toka ng’ambo hivyo kudumaza kabisa uwezo wetu na kutufanya tuendelee kuwa tegemezi
·       Kukosekana kwa mikakati sahihi ya kukuza na kuendeleza teknolojia ambayo imefanya Kushindwa kubadli mafanikio ya tafiti kuwa viwanda (industrialization of applied research); kushindwa kugeuza viwanda kuwa fursa za kibishara ambako ndiko pesa ilipo.
SULUHISHO LETU
Ili kujibu changamoto hizo, jiji la Tanzanite City limeanzishiwa kwa lengo la kuweka mazingira bora ya kukuzwa ubunifu na kuanzishwa kwa viwanda na makampuni.  MAMBO SITA MUHIMU YATAKAYOFANYWA NA TANZANITE CITY
1.     Miundombinu bora  (infrastructures and sound facilities)
2.     Mikakati mahususi ya kukuza vipaji na ubunifu
3.     Upatikanaji wa mitaji na fedha
4.     Upatikanaji wa huduma mbalimbali
5.     Kujenga mfumo madhubuti wa biashara (Adequate business systems);
6.     Kutangaza na kukuza taasisi za wajasiliamali na ujasiliamali (Promotion of SMIEs and entrepreneurship);
JIJI LITAKAVYOFANYA KAZI
Watu wenye vipaji toka kokote kule duniani wataalikwa kushirikiana na vijana wetu wataalam katika fani za Sayansi na teknolojia wanaohitimu vyuo ambao watawekwa kwenye makambi ya teknlojia (classified technology development camps),  katika jiji hili ili waweze kubuni na kujenga uwezo wa kutengeneza bidhaa mbalimbali za kitechnolojia huku wakipewa kila aina ya msaada watakaohitaji, kuanzisha viwanda pamoja na kuanzisha makampuni watakayoyamiliki kwa ushirika na watanzania wengine kupititia Klabu ya marafiki wa Tanzanite City.
Vijana hawa wataalam watapewa mission mahususi za kubuni na kujenga uweza wa kuzalisha teknlojia kulingana na vipaumbele na mahitaji soko, kukopi teknolojia ambazo tayari zipo, kuzifanyia maboresho kulingana na mahitaji ya soko, na kuanzisha bidhaa na teknoljia mpya ambazo ni zetu wenyewe baada ya kuwa tumejenga uwezo wa kutosha.
Lengo ni kujenga uwezo wetu wa ndani wa kuzalisha bidhaa za kiviwanda na kiteknoljia, kwa mfano badala ya kuuza simu toka nchi za Asia, tuunda na kuuza simu zetu wenyewe! Badala ya kuifuata Guangzhou kule Uchina tunataka kujenga Guangzhou yetu hapa hapa nchini
TUNAHITAJI NINI TOKA KWAKO MDAU
Tunawataka wanachi na wadau  wengine kujiunga na klabu ili;
Kwanza waweze kuchangia  kwenye ujenzi wa jiji kwa fedha au mawazo
Pili waweze kushiriki kikamilifu kwenye ujenzi wa Tanzania mpya
Wewe kama mdau muhimu tunakuaomba tuungane na Mh Rais John Pombe Magufuli na mkuu wetu wa Mkoa ambaye pamoja , Wabunge wetu katkia juhudi zao za kuleta maendeleo ya Viwanda na kukuza uchumi wa Mkoa wetu .
TUMEDHARIA KUIFANYA MBEYA KUWA GUANGZHOU YA AFRIKA,






Tanzanite City Chunya Full Council Briefing Part 1



Sehemu ya kwanza ya mkutano wa utambulisho wa Tanzanite City kwa wakuu wa idara na madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Chunya ambako ndiko jiji linajengwa.