Search This Blog

TANZANITE CITY: The Africa's Factory & Innovation Powerhouse!

TANZANITE CITY: The Africa's Factory & Innovation Powerhouse!
We Will Turn Bushes Into Highly Industrialized City

Wednesday, October 11, 2017

KWA NINI TANZANITE CITY NI MUHIMU KWA MAPINDUNZI YA VIWANDA TANZANIA!!!

DHUMUNI KUU
Tanzanite City ni jiji la sayansi, teknolojia na ubunifu ambalo lipo njiani kujengwa mkoani Mbeya katka wilaya ya Chunya. Jiji hili linajengwa kwa ushirikiano kati ya ESTA-TZ na ofisi ya mkuu wa mkoa, Mh. Amos Makalla, ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Chunya, Mkurugenzi na Balaza la Madiwani wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya.
Lengo kuu la kuanzishwa kwa Tanzanite City ni kujenga uwezo wa taifa letu kwenye mambo ya teknolojia na kuhamasisha mapinduzi ya viwanda yatakayoifanya Tanzania kuwa kiwanda cha Afrika na kitovu cha ubunifu katika ukanda huu wa Afrika kusini mwa jangwa la Sahara.
Jiji hili litasaidia kuwajengea uwezo wa ubunifu katika maswala teknolojia, vijana wanaomaliza vyuo katika fani za sayansi na teknolojia, na kuwawezesha kuanzisha viwanda na kuunda makampuni watakayo yaendesha kwa ubia na wanachi wengine, kupitia klabu ya marafiki wa Tanzanite City
BAADHI YA CHANGAMOTO TUNAZOKWENDA KUZIJIBU
Kama tujuavyo serikali yaawamu ya tano ya  Mh. John Pombe Magufuli imedhamiria kuipeleka Tanzania kwenye uchumi wa viwanda, Lakini katika safari hiyo kuna changamoto kadhaa ambazo ni lazima  zifanyiwe kazi.
·       Mazingira magumu na yasiyo rafiki yanayoyoua utamaduni wa kuwekeza katika viwanda yanawafanya watanzania wengi kuagiza bidhaa za viwanda toka nje,
·       Kukosekana kwa kiunganishi kati ya wanjasiriamali wazawa na wawekezaji wa nje kunakotokana na tofauti kubwa sana katika technoljia. Tofauti hii imefanya kuwa vigumu sana kwa wazawa kuweza kuhamisha teknolojia toka ng’ambo hivyo kudumaza kabisa uwezo wetu na kutufanya tuendelee kuwa tegemezi
·       Kukosekana kwa mikakati sahihi ya kukuza na kuendeleza teknolojia ambayo imefanya Kushindwa kubadli mafanikio ya tafiti kuwa viwanda (industrialization of applied research); kushindwa kugeuza viwanda kuwa fursa za kibishara ambako ndiko pesa ilipo.
SULUHISHO LETU
Ili kujibu changamoto hizo, jiji la Tanzanite City limeanzishiwa kwa lengo la kuweka mazingira bora ya kukuzwa ubunifu na kuanzishwa kwa viwanda na makampuni.  MAMBO SITA MUHIMU YATAKAYOFANYWA NA TANZANITE CITY
1.     Miundombinu bora  (infrastructures and sound facilities)
2.     Mikakati mahususi ya kukuza vipaji na ubunifu
3.     Upatikanaji wa mitaji na fedha
4.     Upatikanaji wa huduma mbalimbali
5.     Kujenga mfumo madhubuti wa biashara (Adequate business systems);
6.     Kutangaza na kukuza taasisi za wajasiliamali na ujasiliamali (Promotion of SMIEs and entrepreneurship);
JIJI LITAKAVYOFANYA KAZI
Watu wenye vipaji toka kokote kule duniani wataalikwa kushirikiana na vijana wetu wataalam katika fani za Sayansi na teknolojia wanaohitimu vyuo ambao watawekwa kwenye makambi ya teknlojia (classified technology development camps),  katika jiji hili ili waweze kubuni na kujenga uwezo wa kutengeneza bidhaa mbalimbali za kitechnolojia huku wakipewa kila aina ya msaada watakaohitaji, kuanzisha viwanda pamoja na kuanzisha makampuni watakayoyamiliki kwa ushirika na watanzania wengine kupititia Klabu ya marafiki wa Tanzanite City.
Vijana hawa wataalam watapewa mission mahususi za kubuni na kujenga uweza wa kuzalisha teknlojia kulingana na vipaumbele na mahitaji soko, kukopi teknolojia ambazo tayari zipo, kuzifanyia maboresho kulingana na mahitaji ya soko, na kuanzisha bidhaa na teknoljia mpya ambazo ni zetu wenyewe baada ya kuwa tumejenga uwezo wa kutosha.
Lengo ni kujenga uwezo wetu wa ndani wa kuzalisha bidhaa za kiviwanda na kiteknoljia, kwa mfano badala ya kuuza simu toka nchi za Asia, tuunda na kuuza simu zetu wenyewe! Badala ya kuifuata Guangzhou kule Uchina tunataka kujenga Guangzhou yetu hapa hapa nchini
TUNAHITAJI NINI TOKA KWAKO MDAU
Tunawataka wanachi na wadau  wengine kujiunga na klabu ili;
Kwanza waweze kuchangia  kwenye ujenzi wa jiji kwa fedha au mawazo
Pili waweze kushiriki kikamilifu kwenye ujenzi wa Tanzania mpya
Wewe kama mdau muhimu tunakuaomba tuungane na Mh Rais John Pombe Magufuli na mkuu wetu wa Mkoa ambaye pamoja , Wabunge wetu katkia juhudi zao za kuleta maendeleo ya Viwanda na kukuza uchumi wa Mkoa wetu .
TUMEDHARIA KUIFANYA MBEYA KUWA GUANGZHOU YA AFRIKA,