Search This Blog

TANZANITE CITY: The Africa's Factory & Innovation Powerhouse!

TANZANITE CITY: The Africa's Factory & Innovation Powerhouse!
We Will Turn Bushes Into Highly Industrialized City

Tuesday, December 3, 2013

Tunawezaje kufaidika na uingizaji teknolojia toka ng’ambo?

Maendeleo ya  kitenolojia ni moja ya nguzo kuu muhimu sana katika taifa katika kuongeza ufanisi wa uzalishaji, kupunguza upotevu na kuongeza ubora wa bidhaa, pamoja na kuongeza ushindani katika sekta husika. Jambo moja kubwa na la msingi katika kudumisha ushindani ni uwezo wa washindani kubadilika haraka kuendana na mabadiliko ya mahitaji ya soko la kimataifa.
Tunaweza kuuelezea uwezo wa taifa kiteknolojia katika ngazi kuu tatu ambazo ni: mosi ni uwezo wa kutunza na kuendesha mitambo ya uzalishaji iliyonunuliwa toka ng’ambo; pili ni uwezo wa kunakili au kukopi na kufanya marekebisho muhimu ili mitambo iliyonakiliwa iweze kuendana na mahitaji na mazingira ya mahali inapotarajiwa kutumika; tatu ni uwezo wa kubuni na kusanifu mitambo au mifumo ya uzalishaji na vifaa vya uzalishaji.
Maendeleo hayo ya teknolojia yanaongozwa na weledi wa kiubunifu katika uvumbuzi wa bidhaa mpya na kuzifikisha sokoni. Ili kuweza kuwa na weledi wa ubunifu na namna ya kufikisha sokoni bidhaa hizo mpya kunahitajika kufanyika kwa utafiti wa kina na majaribio mengi ya kisayansi (experimentation), ujuzi, motisha na sapoti ya kitaasisi kuweza kupeleka bidhaa sokoni. Pamoja na kuwa mfumo rasmi wa kujenga weledi unalenga tafiti na ubunifu katika mfumo ulio rasmi zaidi, unahusisha pia majaribio yanye msingi wa kimasoko na kimatumizi kwa lengo la kuelewa walaji wanahitaji nini. Utengenezaji na upelekaji sokoni wa bidhaa hizo pia unaweza kufanywa katika mifumo yote ulio rasmi na usio reasmi.
Namna ambavyo teknolojia inaweza kuingizwa inchini
Kuna namna nyingi ambazo taifa linaweza kuingiza teknolojia mpya toka nje ikiwa ni pamoja na biashara za kawaida za uagizaji wa bidhaa za kiteknolojia toka nje nchi, mikataba ya ruhusa ya kutumia kiteknolojia (licensing of technology); kuchangia teknolojia (sharing of designs), haki miliki (patents), kanuni (formulae), ubia kwenye miradi mikubwa ya teknolojia ya juu, (high-tech joint ventures); kusomesha wataalam nje ya nchi; ushirikiano kwenye mambo ya msingi ya ubunifu na uendaelezaji teknolojia (collaboration in basic and/or innovative research and development); pamoja na misaada ya kiteknolojia (donated technologies, machinery, or equipment). Vile vile kuna njia ambazo ni kinyume cha uungwana, hizi pia zinaweza kuwa  kupewa mamlaka ya kuingiza teknolojia kwa kubadilishana na soko; kutumia teknolojia kinyume na makubaliano ya msingi ya uingizaji wa teknolojia husika, wizi au kugushi makabrasha ya teknolojia (theft or infringement of intellectual property) na kuchunguza kwa siri teknolojia za wengine (espionage)
Lengo kuu na la msingi la kuingiza teknolojia ni kupata manufaa ya kiuchumi (economic gain) iwe ni ya muda mfupi au muda mrefu. Kwa ujumla hamasa kubwa ni (i) kuinginza nchini teknolojia mhimu na sahihi ambazo hazipatikani ndani ya nchi, na (ii) kujenga uwezo wa ndani kiteknolojia katika eneo mahususi au sekta kupitia uzalishaji, uhandisi au ubunifu katika teknolojia zinazoingizwa nchini.
Serikari na wadau ni lazima kuhimiza kuingizwa nchini kwa weledi/ujuzi na taarifa za kisayansi na kiteknolojia kutoka nchi zilizoendelea, pia tuhimize umuhimu wa kueneza na kuhakisha kuwa teknolojia zote zinazoingia nchini zinapelekea kukua kwa teknolojia zetu na kuhama kutoka teknlojia za hali ya chini “low-tech”na kuelekea kwenye teknloljia za hali ya juu  “high-tech.” badala ya kuzalisha vitu vidogovidogo kama mabatiki mishumaa sabuni n.k.  tuanze kuzalisha vitu kama kompyuta, magari simu za kisasa, meli, ndege n.k.
Ni lazima tuweke mkazo mkubwa sana kwenye uwezeshaji wa wajasiliamali wetu wakubwa na wadogo ili waweze kuzalisha bidhaa bora za kiteknolojia zitakazoweza kukushindana vilivyo katika soko la ndani na la nje, hivyo kuongeza ajira na kukuza uchumi
Yatupasa sasa tujipange kwa mikakati madhubuti ya kuhakisha kuwa wajasilia mali wetu wadogo na wakati ndiyo wanakuwa kiini cha utafiti wa kiteknolojia na ubunifu wa bidhaa bora kabisa, serikari na taasisi zake zijenge madaraja baina yao na wajasiliamali wazalendo ili waweze kupata fursa ya kutumia miundo mbinu iliyopo nchini kwa manufaa ya maendeleo ya taifa letu, ni lazima sasa tuwahamasishe wajasiliamali wetu wa Tanzania kujikita katika kuzielewa na kuzitumia ipasavyo teknolojia zinazoingia nchini badala ya kuangalia zaidi faida ya haraka haraka kutokana na teknolojia zinzoingia hapa nchini, tujikite katiaka kuingiza nchini teknolojia sahihi ambazo hazipatikani hapa kwetu na ambazo ni mwafaka kwa maendeleo yetu, lakini pia tusisahau kusomesha vijana wngi zaidi na kuliandaa taifa kwa kuwa na wafanyakazi wa kutosha wenye ujuzi na owezo wa kukabiliana na changamoto za maendeleo ya teknolojia, tuwaanda vijana wetu kuwa wanasayansi wa kesho, mafundi, madaktari n.k.
Ili tuweze kufaninikiwa katika hili tunapaswa kufanya uwekezaji mkubwa kwenye teknolojia ili mwisho wa siku vijana tutakaokuwa tumeasomesha wasije wakakosa sehemu za kuutumia weledi na ujuszi wao, vilevile ni lazima tuwe na mkakati wa kuhakiksha wataalam wote wenye vipaji maalum hawandoki nchini kwa kuwatengenezea mazingira bora ya wao kutumia vipaji vyao kwa manufaa ya taifa huku na wao wakifaidika na matunda ya juhudi zao jambo litakalowafanya waione haja ya kutimkia nje ya nchi mara tu wanapomaliza masomo yao ya juu
Tujenge uwezo wa kuzielewa na kuzitumia kwa ubunifu teknolojia zinazoingia nchini kwakuweka mkakati wa makusudi wa kuwa saidia wajasiliamali wanashughulika na teknolojia kwa kuwapunguzia urasimu wa kupata mikopo katika mabenki, taasisi za kutoa huduma kama TFDA, TRA, Na kwingineko kama wanavyofanyiwa wawekzaji wa kigeni, wasamehewe kodi ili viwanda vyao viwekeze zaidi kwenye utafiti na maendeleo ya teknolojia, wapewe rasilimali ambazo haziligharimu chochote taifa kama vila ardhi bila masharti makubwa ili iwasaidie katika kukua na kuwekeza, kama hayo yanawezekana kwa wgeni sioni kwanini yashindikane kwa wananchi wetu wenyewe, serikari itenge kila wilaya nchini eneo maalum la ardhi kwa ajili ya uwekezaji wa ndani wa wajasiliamali katika teknolojia, walau kila mkoa uwe na kituo kikubwa cha kiashara “business park” ambapo wajasiliamali watauzia bidhaa zao na kuwa kama sehemu ya maonyesho ya kitknolojia na kuwakutanisha wajasiliamali mbalimbali na wateja wao na kuwa kitua cha taarifa za kisayansi na teknolojia
Mikiakati yetu ni lazima ilenge katika kuwa na viwanda vingi vidogovidogo vya uzalishaji bidhaa mbalimbali kuanzia vifaa vidogovidogo vya elektroniki hadi kompyuta za hali ya juu kabisa, teknolojia ya habari, usafiri wa anga, maji na barabara. Tupo nyuma lakini hatujachelewa, tuanze sasa tutafika tu!!!

No comments:

Post a Comment