Search This Blog

TANZANITE CITY: The Africa's Factory & Innovation Powerhouse!

TANZANITE CITY: The Africa's Factory & Innovation Powerhouse!
We Will Turn Bushes Into Highly Industrialized City

Sunday, October 15, 2017

Tanzanite City Chunya Full Council Briefing Part 3



Sehemu ya tatu ya mkutano wa utambulisho wa Tanzanite City kwa wakuu wa idara na madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Chunya ambako ndiko jiji linajengwa.

Saturday, October 14, 2017

TANZANITE CITY; FURSA MPYA NA MBEYA MPYA, KUELEKEA TANZANIA YA VIWANDA

Mpango wa ujenzi wa jiji la sayansi, teknolojia na ubunifu katika wilaya ya  Chunya mkoani Mbeya unatoa fursa nyingine ya kiuchumi kwa watanzania na wakaazi wa mkoa wa Mbeya.  Katika wakati ambapo nchi yetu ipo kwenye kipindi cha mpito kuelekea uchumi wa kati na wa viwanda, mkoa wa Mbeya chini ya uongozi wa Mh. Amosi Makalla kwa kushirikiana kampuni ya ESTA-TZ na uongozi mzima wa wilaya na halmashauri ya wilaya ya Chunya umeanzisha mpango maalum wa kuifanya Mbeya kuwa kitovu cha maendeleo ya teknolojia na mapinduzi ya viwanda katika bara letu la Africa kusini mwa jangwa la sahara.
Katika mpango huu ambao eneo la kuanzia, kiasi cha kilomita za mraba miatano (500sqKm) katika wilaya ya Chunya, litatumika kujenga jiji la Tanzanite. Lengo kuu likiwa ni kuondoa utegemezi wa taifa letu kwa bidhaa na teknolojia mabalilmbali toka nje ya nchi. Katika kipindi cha miaka kumi na tano ijayo Tanzanite city inatarajiwa kujenga uwezo wa taifa letu katika ubunifu wa teknolojia na uzalishaji wa viwandani.
Ili kufikia lengo ambalo mkoa wa Mbeya umejiwekea kufikia mwaka 2030, mkakati mahsusi umewekwa wa kuwekeza kwa Vijana wenye vipaji wanaohitimu kutoka katika taasisi zetu za elimu ya juu.  Pindi wanapohitimu masomo yao, Vijana hao watakuwa wanawekwa kwenye makambi maalumu ya teknlolojia ndani ya jiji la Tanzanite, ambako huko watapewa kila kitu wanachohitaji kuweza kujenge uwezo katika masuala ya ubunifu wa teknolojia na uzalishaji. Vijana hawa watakuwa wanapatiwa mafunzo maalumu ya kuwawezesha kuanzisha na kuendeleza viwanda vitakavyotokana na kazi za kibunifu watakazokuwa wanazifanya makambini.
Mpango huu utawawezesha wazawa wote bila kujali mazingira wanayotoka au asili ya mtu, kuweza kumiliki viwanda kwa pamoja na vijana wabunifu ambao ndiyo watakuwa wakurugenzi wa makampuni hayo yatakayoundwa. Hadi sasa kuna maeneo zaidi ya mia tatu (300 Technology development missions) ambayo yapo tayari kuanza kufanyiwa kazi na vijana pindi ujenzi wa awali wa miundo mbinu muhimu utakapokamilika. Inatarajiwa kwamba maandalizi ya awali ya ujenzi wa Tanzanite City yatakamilika mwishoni mwa robo ya kwanza mwakani (March 2018) ambapo jiji litaanza rasmi shughuli zake.
Miezi sita baadaye viwanda visivyopungua 60 vitaanzishwa na kutoa ajira za moja kwa moja kiasi cha 1200. Baada ya hapo kila wiki kutakuwa na viwanda vipya vinaanzishwa na idadi yake itakuwa ikiongezeka siku hadi siku ambapo katika miaka 15 hadi 2030 jumla makmpuni  54,600 yanatarajiwa kuanzishwa na kutoa ajira za moja kwa moja zisozopungua milioni mbili na nusu.
Tafiti zinaonyesha kuwa kila ajira moja rasmi inazalisha ajira kati ya tatu hadi tano zisizokuwa rasmi. Hivyo katika kipindi cha miaka kumi na tano ijayo Tanzanite City itaweza kuzalisha ajira kwa watu wanaokaribia milioni saba. Sehemu kubwa ya watu hawa pamoja na familia zao watakuwa wanaishi ndani ya wilaya ya Chunya na maeneo jirani katika mikoa ya Songwe na Mbeya. Idadi hii ya watu itahitaji miundombinu mbalimbali ambayo Tanzanite City imejiandaa kikamilifu kuijenga kwa kushirikiana na marafiki pamoja na wadau wetu wote wa maendeleo katika mkoa wa Mbeya.
Tanzanite City inaleta fursa ya kipekee kwa wakazi wa Mbeya, na watanzania wote kwa ujumla, kwani kupitia klabu ya marafiki wa Tanzanite City kila mwanzanchi Mtanzania ataweza kushiriki kwa namna moja au nyingine katika kujenga uchumi wa viwanda. Lakini pia kupitia klabu ya marafiki wa Tanzanite City, watoto wa watanzania masikini wataweza kupata fursa ya kutumia vipaji vyao kubuni teknolojia na kuanzisha makampuni watakayoyamiliki kwa pamoja na watanzania wengine ambao pia ni wanachama wa klabu. Jambo hili lisingewezekana bila ya Tanzanite City. Kwa utaratibu huu hakuna mtanzania atakayeachwa nje ya uchumi wa viwanda kama atakuwa mwanachama wa klabu isipokuwa kwa mapenzi yake mwenyewe!
Klabu ya marafiki wa Tanzanite City ni chombo muhimu sana kwa ujenzi wa jiji la Tanzanite na uchumi wa viwanda kama tunavyotaka kwa sababu kuu mbilli; moja ni kuwa, klabu ndiyo njia pekee ya uhakika itakayowaunganisha watanzania wote na kuwapatia fursa ya kushiriki kikamilifu katika ujenzi wa Tanzania ya viwanda kama wadau na wamiliki. Pili, klabu kupitia michango na ada za wanachama ni chanzo muhimu cha mapato yatakayowezesha kugharimia shughuli na miradi mbalimbali ya ujenzi wa jiji na uendelezaji teknolojia. Wananchi kupitia klabu watafaidika na fursa nyingi sana zitakazotokana na ujenzi wa jiji hili hasa katika maeneo ya miundombinu, na huduma.
Kwa kuzingatia kuwa jiji la Tanzanite litakuwa kiwanda na kitovu cha mapinduzi ya viwanda na maendeleo ya teknlojia katika ukanda huu wa maziwa makuu ya Afrika, watu kutoka mataifa mbalimbali ya afrika watakuja Mbeya aidha kama watalii, wawekezaji ama wafanya biashara, hivyo kupelekea kuwa na fursa nyingi sana, baadhi nimeziorodhesha hapa:
1.         Huduma;
Usafiri na usafirishaji wa watu na mizigo, huduma za hoteli na mikahawa, huduma za afya, elimu ya msingi, secondary na vyuo (mahitaji ya vyuo ni makubwa kiasi cha kuhitajika vyuo zaidi 16 vitavyo toa kozi maalumu zinazoendana na mahitaji ya shughuli za Tanzanite City), ukusanyaji wa taka ngumu, huduma za ulinzi na usalama, huduma za simu na data, n.k.
2.         Miundombinu
Ujenzi wa barabara, mitandao ya maji safi na maji taka, uzalishaji na usambazaji wa umeme, mawasiliano, n.k.
3.         Ujenzi wa nyumba
Nyumba za kuishi, majengo ya biashara, ofisi na viwanda
4.         Biashara
Bima, mabenki, maduka makubwa (Malls), wasambazaji wa bidhaa zinazozalishwa ndani ya jiji, wauzaji wa bidhaa kwa matumizi ya nyumbani kama vyakula na vifaa vingine, sehemu za burudani, n.k.
Ili mtu aweze kunufaika na fursa hizo, ni sharti awe mwanachama wa klabu ya marafiki wa Tanzanite City, kwa maana nyingine anatakiwa kuwa RAFIKI wa Tanzanite City. Rafiki wa kweli ni mtu ambaye yupo tayari kujitoa kwa kila hali kwa ajili ya manufaa ya rafiki yake hata kama yeye mwenyewe hafaidiki moja kwa moja na kujitoa huko. Marafiki wa Tanzaite City watakuwa tayari kuichangia Tanzanite City kwa kulipia ada zao za uwanachama kwa wakati ili kuwawezesha vijana wa watanzania kutimiza ndoto zao na kuigeuza dunia kuwa wanachotaka. Kupitia klabu hii siyo lazima kuwa kila utakachochangia lazima kikunufaishe, mchango wako utakuwezesha kuwa miongoni mwa wadau watakoweza kunufaika na fursa ambazo michango yanu kama marafiki itakuwa imetumika kuzitengeneza kupita vijana wetu wenye vipaji watakaokuwa makambini.
Ni wazi kuwa sasa wanachi wa mkoa wa Mbeya na watanzania wangine wote tunapaswa kumuunga mkono mkuu wa mkoa Mh. Amosi Makalla, mkuu wa wilaya na uongozi mzima wa halmashauri ya wilaya ya Chunya, kwa kujiunga na klabu ya marafiki wa Tanzanite City ili tuweze kushiriki kikamilifu kutengeneza fursa za kiuchumi zitakauzo tufaidisha watanzania wote kwa maendeleo ya wote!  


Thursday, October 12, 2017

Tanzanite City Chunya Full Council Briefing Part 2



Sehemu ya pili ya mkutano wa utambulisho wa Tanzanite City kwa wakuu wa idara na madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Chunya ambako ndiko jiji linajengwa.

Wednesday, October 11, 2017

KWA NINI TANZANITE CITY NI MUHIMU KWA MAPINDUNZI YA VIWANDA TANZANIA!!!

DHUMUNI KUU
Tanzanite City ni jiji la sayansi, teknolojia na ubunifu ambalo lipo njiani kujengwa mkoani Mbeya katka wilaya ya Chunya. Jiji hili linajengwa kwa ushirikiano kati ya ESTA-TZ na ofisi ya mkuu wa mkoa, Mh. Amos Makalla, ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Chunya, Mkurugenzi na Balaza la Madiwani wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya.
Lengo kuu la kuanzishwa kwa Tanzanite City ni kujenga uwezo wa taifa letu kwenye mambo ya teknolojia na kuhamasisha mapinduzi ya viwanda yatakayoifanya Tanzania kuwa kiwanda cha Afrika na kitovu cha ubunifu katika ukanda huu wa Afrika kusini mwa jangwa la Sahara.
Jiji hili litasaidia kuwajengea uwezo wa ubunifu katika maswala teknolojia, vijana wanaomaliza vyuo katika fani za sayansi na teknolojia, na kuwawezesha kuanzisha viwanda na kuunda makampuni watakayo yaendesha kwa ubia na wanachi wengine, kupitia klabu ya marafiki wa Tanzanite City
BAADHI YA CHANGAMOTO TUNAZOKWENDA KUZIJIBU
Kama tujuavyo serikali yaawamu ya tano ya  Mh. John Pombe Magufuli imedhamiria kuipeleka Tanzania kwenye uchumi wa viwanda, Lakini katika safari hiyo kuna changamoto kadhaa ambazo ni lazima  zifanyiwe kazi.
·       Mazingira magumu na yasiyo rafiki yanayoyoua utamaduni wa kuwekeza katika viwanda yanawafanya watanzania wengi kuagiza bidhaa za viwanda toka nje,
·       Kukosekana kwa kiunganishi kati ya wanjasiriamali wazawa na wawekezaji wa nje kunakotokana na tofauti kubwa sana katika technoljia. Tofauti hii imefanya kuwa vigumu sana kwa wazawa kuweza kuhamisha teknolojia toka ng’ambo hivyo kudumaza kabisa uwezo wetu na kutufanya tuendelee kuwa tegemezi
·       Kukosekana kwa mikakati sahihi ya kukuza na kuendeleza teknolojia ambayo imefanya Kushindwa kubadli mafanikio ya tafiti kuwa viwanda (industrialization of applied research); kushindwa kugeuza viwanda kuwa fursa za kibishara ambako ndiko pesa ilipo.
SULUHISHO LETU
Ili kujibu changamoto hizo, jiji la Tanzanite City limeanzishiwa kwa lengo la kuweka mazingira bora ya kukuzwa ubunifu na kuanzishwa kwa viwanda na makampuni.  MAMBO SITA MUHIMU YATAKAYOFANYWA NA TANZANITE CITY
1.     Miundombinu bora  (infrastructures and sound facilities)
2.     Mikakati mahususi ya kukuza vipaji na ubunifu
3.     Upatikanaji wa mitaji na fedha
4.     Upatikanaji wa huduma mbalimbali
5.     Kujenga mfumo madhubuti wa biashara (Adequate business systems);
6.     Kutangaza na kukuza taasisi za wajasiliamali na ujasiliamali (Promotion of SMIEs and entrepreneurship);
JIJI LITAKAVYOFANYA KAZI
Watu wenye vipaji toka kokote kule duniani wataalikwa kushirikiana na vijana wetu wataalam katika fani za Sayansi na teknolojia wanaohitimu vyuo ambao watawekwa kwenye makambi ya teknlojia (classified technology development camps),  katika jiji hili ili waweze kubuni na kujenga uwezo wa kutengeneza bidhaa mbalimbali za kitechnolojia huku wakipewa kila aina ya msaada watakaohitaji, kuanzisha viwanda pamoja na kuanzisha makampuni watakayoyamiliki kwa ushirika na watanzania wengine kupititia Klabu ya marafiki wa Tanzanite City.
Vijana hawa wataalam watapewa mission mahususi za kubuni na kujenga uweza wa kuzalisha teknlojia kulingana na vipaumbele na mahitaji soko, kukopi teknolojia ambazo tayari zipo, kuzifanyia maboresho kulingana na mahitaji ya soko, na kuanzisha bidhaa na teknoljia mpya ambazo ni zetu wenyewe baada ya kuwa tumejenga uwezo wa kutosha.
Lengo ni kujenga uwezo wetu wa ndani wa kuzalisha bidhaa za kiviwanda na kiteknoljia, kwa mfano badala ya kuuza simu toka nchi za Asia, tuunda na kuuza simu zetu wenyewe! Badala ya kuifuata Guangzhou kule Uchina tunataka kujenga Guangzhou yetu hapa hapa nchini
TUNAHITAJI NINI TOKA KWAKO MDAU
Tunawataka wanachi na wadau  wengine kujiunga na klabu ili;
Kwanza waweze kuchangia  kwenye ujenzi wa jiji kwa fedha au mawazo
Pili waweze kushiriki kikamilifu kwenye ujenzi wa Tanzania mpya
Wewe kama mdau muhimu tunakuaomba tuungane na Mh Rais John Pombe Magufuli na mkuu wetu wa Mkoa ambaye pamoja , Wabunge wetu katkia juhudi zao za kuleta maendeleo ya Viwanda na kukuza uchumi wa Mkoa wetu .
TUMEDHARIA KUIFANYA MBEYA KUWA GUANGZHOU YA AFRIKA,






Tanzanite City Chunya Full Council Briefing Part 1



Sehemu ya kwanza ya mkutano wa utambulisho wa Tanzanite City kwa wakuu wa idara na madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Chunya ambako ndiko jiji linajengwa.

Sunday, October 8, 2017

TANZANITE CITY YASHIRIKI VILIVYO KATIKA JUKWAA LA UWEKEZAJI MBEYA


Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mh. Amos Makalla wakisalimiana na Nsollo Nkalla ambaye ni mwenyekiti wa Steering Committee ya mradi wa ujenzi wa Tanzanite City-Chunya, nje ya ukumbi baada ya kongamano liliandaliwa na mkuu wa mkoa kwa ajiri ya kutangaza fursa za kiuchumi na kuvutia watu kuwekeza mkoani Mbeya.

Salaam za pongezi kwa Mh. Dr. Mary Mwanjelwa (Naibu Waziri Mteule wa Kilimo)


Mheshimiwa Dr. Mary Mwanjelwa, Naibu Waziri Mteule Wa Kilimo

Kamati ya uongozi inayoshugulikia ujenzi wa jiji la sayansi, teknolojia na ubunifu la Tanzanite City – Chunya, pamoja na wadau wetu wote kupitia klabu ya marafiki wa Tanzanite City, tunapenda kutoa pongezi zetu za dhati kabisa kwa mbunge wetu wa Mbeya na mdau wa Tanzanite City, Mheshimiwa Dr. MARY MWANJELWA kwa kuteuliwa kwake na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. John Pombe Magufuli Kuwa Naibu Waziri wa Kilimo.
Tunatambua uwezo mkubwa sana alionao Mh. Mwanjelwa katika kutekeleza majukumu yake. Sisi kama wadau wa maendeleo ya viwanda na Teknolojia tunatambua jukumu kubwa na zito analokwenda kulibeba Mh Mwanjelwa, si mchezo-mchezo bali anatakiwa kuwa mbunifu sana na asiyechoka kujifunza. Nchi yetu ni kubwa sana na ina matatizo mengi mno yanayohusiana na wizara anayokwenda kuifanyia kazi.
Moja ya changamoto ambazo Mh. Naibu Waziri atakutana nazo katika utekelezaji wa majukumu yake ni matumizi duni ya teknolojia katika kilimo kwa ujumla wake na namna ya kuongeza thamani ya mazao ya kilimo. Katika wakati huu ambao taifa letu lipo kwenye kipindi cha mpito kuelekea uchumi wa kiviwanda, suala la teknolojia linapaswa kupewa kipaumbele kwani linagusa kila Nyanja ya kilimo, kuanzia kwenye maandalizi ya ardhi ikiwa ni pamoja na kuilima, kupanda na kupandikiza mazao mashambani, kutunza mazao yaliyoshambani ili yaweze kutoa matunda bora na ya kutosha, uvunaji wa mazao na kuyasafirisha toka mashambani, uhifadhi wa mazao ghafi ya kilimo pamoja na kuyaongezea thamani. Yote hayo yanahitaji teknolojia kwa mapana yake!
Mh. Naibu Waziri, ni vigumu sana kuweza kuendelea kama taifa, iwe ni kwenye kilimo, viwanda au hata biashara tu, iwapo tutapuuza matumizi ya teknolojia. Lakini pamoja na kutilia maanani matumizi hayo ya teknolojia, bado hatutaweza kufikia malengo yetu ya kiuchumi kama tutaendelea kuwa tegemezi kwa kiteknolojia toka nje. Kwani hao tunaowategemea wao pia wanavyo viapaumbele vyao ambavyo siyo lazima vifanane na vyetu. Hivyo sasa ni jukumu letu kama kweli tunataka kwenda kwenye uchumi wa kati, wa viwanda na kilimo cha kibiashara na chenye tija, kuanza sasa kujenga uwezo wetu wenyewe kwenye mambo ya technolojia ambao ndiyo mhimili wa hivyo viwanda na hicho kilimo tunachokitaka.
Mh. Naibu Waziri, sisi tumeanza na Tanzanite City, ni safari ngumu na ndefu, lakini tumedhamiria kufika mwisho, tunaamini kuwa, kwa kuwekeza kwenye vipaji vya vijana wetu, na kuwasaidia kutimiza ndoto zao, tutabadilisha mustakabari wa taifa letu na kuboresha sana kilimo chetu, tukishirikiana sisi wanachi, wadau wa maendeleo, pamoja na serikali tunaweza kuifanya Tanzania kuwa kiwanda cha Afrika, na kitovu cha ubunifu katika maswala ya teknolojia.
Mh. Naibu Waziri, tuna jua NIA UNAYO, SABABU UNAYO NA UWEZO UNAO! Tunakuahidi ushirikiano wetu, tunakuombea afya njema, hekima, na heshima kwa watu unaowaongoza, wengi wamepita na hawajaacha alama yoyote baada ya wao kuondoka, na wewe hutaishi milele kwenye hiyo nafasi, lakini tunatamani kuona alama za kazi zako zikidumu daima kwa vizazi vingi vijavyo!! TUNAJUA NA TUNAAMINI UNAWEZA!!! Tuna kutakia kila lililo la heri, ufanikiwa katika majukumu yako hayo kwa taifa letu, MUNGU Akubariki na akulinde siku zote za maisha yako. Amina.

Wednesday, August 2, 2017



Picha za baadhi ya maeneo ya wilaya ya Chunya ilioko mkoani Mbeya ambako mji wa kisayansi wa Tanzanite City unatarajiwa kujengwa.
Picha ya pamoja baada ya kikao cha utambulisho wa Tanzanite City kilichohudhuriwa na mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Chunya,mwenyekiti wa baraza la madiwani pamoja na madiwani wa halmashauri ya Chunya.

Monday, November 21, 2016

LETTER TO HIS EXCELLENCY PRESIDENT DR. JOHN POMBE MAGUFULI

Dear Mr. President,
ESTA-TZ Limited is dealing with the development of a city of science, technology and innovation, I.e. ESTA-Tanzanite City. The City is our endeavor to stimulate the development of home grown technology capabilities by empowering and enabling university and college graduates in the fields of science and technology, to develop technology and manufacturing capabilities, then assist them to launch and build new technology-based industries that will be owned in partnership with other citizen through Friend’s Club of the Tanzanite City
Our motivation being to make the city an Africa’s factory and innovation powerhouse, that will affect everyone’s life in this continent and play great role in improving the quality of life, economic growth and protecting our environment, the Tanzanite City, will be the mining of the talents from the brains of our young people and a factory for processing them out into automobiles, ships, computers, processing industries, TVs, mobile phones, etc. it will be the hatchery of technology industries in Tanzania,
Knowing that this is very big undertaking that we can only achieve with the assistance and generosity from all members of our community, the government and non-government Institutions, and that Without these, achieving this mission will not be possible, we are now working to establish a Not for Profit Trust (ESTA-Tanzanite City Trust) that will be responsible to support the whole mission as described in the Grand Concept Manual
Dear Mr. President, with this letter first of all I would like to recognize your effort to transform our country especially with your ambition to make Tanzania highly industrialized in the next ten years. We know how tuff it is to change the mindset of the people and make them believe in what you are doing against their status quo, don’t be discouraged, one day if not now people will understand your language and see what you are looking after, but before we reach there be sure that a lot will happen to either encourage or discourage you. All in all, it needs big heart and a lot sacrifices that already you have demonstrated, we are sure with that spirit of yours we are heading the right direction.
Dear Mr. President, during Mwl. Nyerere’s age, at schools we were taught that for our nation to develop we need four major ingredients; Land, good politics, people and good governance. With changes that had occurred in the world since the end of cold war in the end of 1980s we can now redefine the ingredients of development as; Good governance, technology and nature resources. Good governance is mandatory but must be mixed with either of the two, technology or access to natural resources or both as it is for the highly developed countries. The poorest countries have only one ingredient and they have stuck, fast developing countries have at least two, good governance and technology, or good governance and plenty of natural resources.
Good governance puts the systems in place and brings discipline and makes the people focus on development businesses. Where good governance is blended with technology, the country becomes strong and stable and can access natural resources from other countries. And when the good governance is blended with plenty of natural resources, the countries could properly plan the use of their resources to acquire the technology they need. Having technology or natural resources without good governance normally leads to the violence and unrests caused by scrambles for control among the greedy
Dear Mr. President, you are now transforming our nation towards good governance and discipline, blending it with the plenty of natural resources our country have been endowed, we only need technology to move from where we are to our promise land. With technology, we will be able to sustainably harvest our natural resources, process them and utilize them to bring wealth to our people, with technology we can make our country the Africa Factory where all other African countries will turn to for their various needs instead of going all the way out to other continents. This will be great footstep embracing the dream of the father of our nation of uniting Africa economically
As I have said above, this is a tuff undertaking and required the participation of all stake holders and citizens of this country to make it. You my president alone won’t succeed, you need our support, and your government if they real want to support your vision of industrialized Tanzania, must truly commit themselves to work with big dreamers who have great ideas and want to change this world.
We at ESTA-TZ believe that this country will be developed by our own efforts, our brains and determinations, no one will come from china, from Europe, from Asia or from America to develop us but all of them can render great contribution to our development if we will be able to partner with them and benefit from each other, they need our resources as much as we need their technology, let’s play the right card now for the better future of our nation.
Understanding this all, the Tanzanite City is one of the strategy that will provide sound facilities & infrastructures required to cater the needs of the expected scientific and technological advancement and supporting R&D and other technological operations in the Tanzanite City and provide to the talents and experts, the required resources to support their’ activities and enable them to conduct researches, build new instruments, conduct experiments, and scientifically test their ideas in development of technologies that address social and economic needs of our people, and bridge the gap between need and means; between scientific & engineering challenges and technological innovations needed to overcome them; between laboratory development and demonstration in the field.
To solve our problems and develop the capability to create jobs and increase the flow of foreign currencies into our country, we must greatly reduce our dependence on imported items and instead we should develop the technology capability to manufacture industrial items to carter our own needs and the needs of our neighboring countries, In order to achieve this. The Tanzanite city if successful will address the following issues:
Importing everything while we export less: This not only narrows the opportunity of our nation to create jobs but also drains our foreign currency reserves which by the way we don’t have much because we don’t export much as we import, to combat this, we must continuously and sustainably reduce within specific period of time, our dependence to the import of technology items by developing technology capabilities to manufacturing of our own products rather than selling products from other countries.
Utilized our country’s geographical position to our advantage: Our country is a gate way by which our land locked neighboring countries use for import of their industrial items and exports of raw materials. When they pass by, we join them and go all the way out there to bring things that our young graduates from our universities would have been manufacturing here.
Export of raw materials: Since we do not have technologies for processing our agricultural products and mineral raw materials we export them raw, our neighbors are also using our country to export their raw materials. The question is wouldn’t it be wealth if we could process those materials into finished or semi-finished products before we allow them out of our boarders? What does it take and How do we manage? Where and When should we start? how do we start?   
Lack of access to the new technologies & mechanisms for technology transfer: Now our countries are in competition to lure the foreign investors (FDI) to invest in various manufacturing sectors such as assembling and processing industries. But due to the fact that there is big gap in technology capabilities between the foreign investors and our entrepreneurs and the link between them is very weak, it is difficult for our entrepreneurs gaining access to the new technologies via foreign joint ventures and Foreign Direct Investment hence they are unable to absorb, assimilate, and innovate the new technologies
Because our country has no plenty of resources to facilitate quick evolution industrialization, the best way to go about may involve doing the following:
·         develop our own homegrown technology capabilities and promote rapid progress of export-oriented industrialization and development of strong and competitive Small & Medium Industrial Enterprises as an essential prerequisite for continued development and increased competitiveness of the manufacturing industries.
·         creating geographical proximity between the core industries and its upstream and downstream businesses to easy sharing of the common facilities and resources hence reducing technology development and manufacturing costs, we should create perfect ecosystem and link between economic development, people development and government revenue creation,
·         creating link between foreign investors especially assembly industries and local entrepreneurs especially supporting industries and facilitate innovation driven growth of technology-based industries and finally We need to create conducive environment for launching and building myriad technology-based industries and nurture them through to stand-alone stage, and connect them with foreign investors to create partnership that will benefit both
And that is all about development of the Tanzanite City of Science, Technology and Innovation
Dear Mr. President, May I Take this Opportunity to ask your government to support us and join hands with us to achieving this crucial mission. The generous support of your government will make it possible to develop our own “Guangzhou”, where people from other African countries will turn to for their shopping instead of just passing by and going all the way to Asia buying items that we could manufacture here so creating jobs and increasing our foreign currencies reserve.
From your government, we need two things; number one is land - about 400sqkm with expansion provision for the development of the city where about 100,000 industrial enterprises will be built in the next 15 year that will create about two million direct jobs in this city. Second is support from your governments institution such as COSTECH, TIRDO, SIDO, BRELA, TFDA, TBS etc.
With this support, we are sure to TURN BUSHES INTO HIGHLY INDUSTIALISED CITY, and make our own GUANGZHOU & SILICON VALLEY for Africa
Regards
Nsollo Nkalla
CEO & Founder 
ESTA-Tanzanite City
0713253250 / 0752229090