MAKING CHUNYA A HOTBED OF INNOVATION & INDUSTRIAL REVOLUTION
Search This Blog
TANZANITE CITY: The Africa's Factory & Innovation Powerhouse!
Sunday, October 15, 2017
Tanzanite City Chunya Full Council Briefing Part 3
Sehemu ya tatu ya mkutano wa utambulisho wa Tanzanite City kwa wakuu wa idara na madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Chunya ambako ndiko jiji linajengwa.
Saturday, October 14, 2017
TANZANITE CITY; FURSA MPYA NA MBEYA MPYA, KUELEKEA TANZANIA YA VIWANDA
Mpango wa ujenzi wa jiji la sayansi, teknolojia na
ubunifu katika wilaya ya Chunya mkoani
Mbeya unatoa fursa nyingine ya kiuchumi kwa watanzania na wakaazi wa mkoa wa
Mbeya. Katika wakati ambapo nchi yetu
ipo kwenye kipindi cha mpito kuelekea uchumi wa kati na wa viwanda, mkoa wa
Mbeya chini ya uongozi wa Mh. Amosi Makalla kwa kushirikiana kampuni ya ESTA-TZ
na uongozi mzima wa wilaya na halmashauri ya wilaya ya Chunya umeanzisha mpango
maalum wa kuifanya Mbeya kuwa kitovu cha maendeleo ya teknolojia na mapinduzi ya
viwanda katika bara letu la Africa kusini mwa jangwa la sahara.
Katika mpango huu ambao eneo la kuanzia, kiasi cha
kilomita za mraba miatano (500sqKm) katika wilaya ya Chunya, litatumika kujenga
jiji la Tanzanite. Lengo kuu likiwa ni kuondoa utegemezi wa taifa letu kwa
bidhaa na teknolojia mabalilmbali toka nje ya nchi. Katika kipindi cha miaka
kumi na tano ijayo Tanzanite city inatarajiwa kujenga uwezo wa taifa letu
katika ubunifu wa teknolojia na uzalishaji wa viwandani.
Ili kufikia lengo ambalo mkoa wa Mbeya umejiwekea kufikia
mwaka 2030, mkakati mahsusi umewekwa wa kuwekeza kwa Vijana wenye vipaji
wanaohitimu kutoka katika taasisi zetu za elimu ya juu. Pindi wanapohitimu masomo yao, Vijana hao watakuwa
wanawekwa kwenye makambi maalumu ya teknlolojia ndani ya jiji la Tanzanite,
ambako huko watapewa kila kitu wanachohitaji kuweza kujenge uwezo katika
masuala ya ubunifu wa teknolojia na uzalishaji. Vijana hawa watakuwa wanapatiwa
mafunzo maalumu ya kuwawezesha kuanzisha na kuendeleza viwanda vitakavyotokana
na kazi za kibunifu watakazokuwa wanazifanya makambini.
Mpango huu utawawezesha wazawa wote bila kujali mazingira
wanayotoka au asili ya mtu, kuweza kumiliki viwanda kwa pamoja na vijana
wabunifu ambao ndiyo watakuwa wakurugenzi wa makampuni hayo yatakayoundwa. Hadi
sasa kuna maeneo zaidi ya mia tatu (300 Technology development missions) ambayo
yapo tayari kuanza kufanyiwa kazi na vijana pindi ujenzi wa awali wa miundo
mbinu muhimu utakapokamilika. Inatarajiwa kwamba maandalizi ya awali ya ujenzi
wa Tanzanite City yatakamilika mwishoni mwa robo ya kwanza mwakani (March 2018)
ambapo jiji litaanza rasmi shughuli zake.
Miezi sita baadaye viwanda visivyopungua 60 vitaanzishwa
na kutoa ajira za moja kwa moja kiasi cha 1200. Baada ya hapo kila wiki
kutakuwa na viwanda vipya vinaanzishwa na idadi yake itakuwa ikiongezeka siku
hadi siku ambapo katika miaka 15 hadi 2030 jumla makmpuni 54,600 yanatarajiwa kuanzishwa na kutoa ajira
za moja kwa moja zisozopungua milioni mbili na nusu.
Tafiti zinaonyesha kuwa kila ajira moja rasmi inazalisha
ajira kati ya tatu hadi tano zisizokuwa rasmi. Hivyo katika kipindi cha miaka
kumi na tano ijayo Tanzanite City itaweza kuzalisha ajira kwa watu wanaokaribia
milioni saba. Sehemu kubwa ya watu hawa pamoja na familia zao watakuwa wanaishi
ndani ya wilaya ya Chunya na maeneo jirani katika mikoa ya Songwe na Mbeya. Idadi
hii ya watu itahitaji miundombinu mbalimbali ambayo Tanzanite City imejiandaa
kikamilifu kuijenga kwa kushirikiana na marafiki pamoja na wadau wetu wote wa
maendeleo katika mkoa wa Mbeya.
Tanzanite City inaleta fursa ya kipekee kwa wakazi wa Mbeya,
na watanzania wote kwa ujumla, kwani kupitia klabu ya marafiki wa Tanzanite
City kila mwanzanchi Mtanzania ataweza kushiriki kwa namna moja au nyingine
katika kujenga uchumi wa viwanda. Lakini pia kupitia klabu ya marafiki wa
Tanzanite City, watoto wa watanzania masikini wataweza kupata fursa ya kutumia
vipaji vyao kubuni teknolojia na kuanzisha makampuni watakayoyamiliki kwa
pamoja na watanzania wengine ambao pia ni wanachama wa klabu. Jambo hili
lisingewezekana bila ya Tanzanite City. Kwa utaratibu huu hakuna mtanzania
atakayeachwa nje ya uchumi wa viwanda kama atakuwa mwanachama wa klabu isipokuwa
kwa mapenzi yake mwenyewe!
Klabu ya marafiki wa Tanzanite City ni chombo muhimu sana
kwa ujenzi wa jiji la Tanzanite na uchumi wa viwanda kama tunavyotaka kwa
sababu kuu mbilli; moja ni kuwa, klabu ndiyo njia pekee ya uhakika
itakayowaunganisha watanzania wote na kuwapatia fursa ya kushiriki kikamilifu
katika ujenzi wa Tanzania ya viwanda kama wadau na wamiliki. Pili, klabu
kupitia michango na ada za wanachama ni chanzo muhimu cha mapato
yatakayowezesha kugharimia shughuli na miradi mbalimbali ya ujenzi wa jiji na
uendelezaji teknolojia. Wananchi kupitia klabu watafaidika na fursa nyingi sana
zitakazotokana na ujenzi wa jiji hili hasa katika maeneo ya miundombinu, na
huduma.
Kwa kuzingatia kuwa jiji la Tanzanite litakuwa kiwanda na
kitovu cha mapinduzi ya viwanda na maendeleo ya teknlojia katika ukanda huu wa
maziwa makuu ya Afrika, watu kutoka mataifa mbalimbali ya afrika watakuja Mbeya
aidha kama watalii, wawekezaji ama wafanya biashara, hivyo kupelekea kuwa na fursa
nyingi sana, baadhi nimeziorodhesha hapa:
1.
Huduma;
Usafiri na usafirishaji
wa watu na mizigo, huduma za hoteli na mikahawa, huduma za afya, elimu ya
msingi, secondary na vyuo (mahitaji ya vyuo ni makubwa kiasi cha kuhitajika
vyuo zaidi 16 vitavyo toa kozi maalumu zinazoendana na mahitaji ya shughuli za
Tanzanite City), ukusanyaji wa taka ngumu, huduma za ulinzi na usalama, huduma za
simu na data, n.k.
2.
Miundombinu
Ujenzi wa
barabara, mitandao ya maji safi na maji taka, uzalishaji na usambazaji wa umeme,
mawasiliano, n.k.
3.
Ujenzi wa nyumba
Nyumba za
kuishi, majengo ya biashara, ofisi na viwanda
4.
Biashara
Bima, mabenki,
maduka makubwa (Malls), wasambazaji wa bidhaa zinazozalishwa ndani ya jiji, wauzaji
wa bidhaa kwa matumizi ya nyumbani kama vyakula na vifaa vingine, sehemu za
burudani, n.k.
Ili mtu aweze kunufaika na fursa hizo, ni sharti awe
mwanachama wa klabu ya marafiki wa Tanzanite City, kwa maana nyingine anatakiwa
kuwa RAFIKI wa Tanzanite City. Rafiki wa kweli ni mtu ambaye yupo tayari
kujitoa kwa kila hali kwa ajili ya manufaa ya rafiki yake hata kama yeye
mwenyewe hafaidiki moja kwa moja na kujitoa huko. Marafiki wa Tanzaite City
watakuwa tayari kuichangia Tanzanite City kwa kulipia ada zao za uwanachama kwa
wakati ili kuwawezesha vijana wa watanzania kutimiza ndoto zao na kuigeuza
dunia kuwa wanachotaka. Kupitia klabu hii siyo lazima kuwa kila utakachochangia
lazima kikunufaishe, mchango wako utakuwezesha kuwa miongoni mwa wadau
watakoweza kunufaika na fursa ambazo michango yanu kama marafiki itakuwa
imetumika kuzitengeneza kupita vijana wetu wenye vipaji watakaokuwa makambini.
Ni wazi kuwa sasa wanachi wa mkoa wa Mbeya na watanzania
wangine wote tunapaswa kumuunga mkono mkuu wa mkoa Mh. Amosi Makalla, mkuu wa
wilaya na uongozi mzima
wa halmashauri ya wilaya ya Chunya, kwa kujiunga na klabu ya marafiki wa
Tanzanite City ili tuweze kushiriki kikamilifu kutengeneza fursa za kiuchumi
zitakauzo tufaidisha watanzania wote kwa maendeleo ya wote!
Thursday, October 12, 2017
Tanzanite City Chunya Full Council Briefing Part 2
Sehemu ya pili ya mkutano wa utambulisho wa Tanzanite City kwa wakuu wa idara na madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Chunya ambako ndiko jiji linajengwa.
Wednesday, October 11, 2017
KWA NINI TANZANITE CITY NI MUHIMU KWA MAPINDUNZI YA VIWANDA TANZANIA!!!
DHUMUNI KUU
Tanzanite City ni jiji la sayansi, teknolojia na ubunifu ambalo
lipo njiani kujengwa mkoani Mbeya katka wilaya ya Chunya. Jiji hili linajengwa kwa ushirikiano kati ya ESTA-TZ na ofisi ya mkuu wa mkoa, Mh. Amos Makalla, ofisi
ya Mkuu wa Wilaya ya Chunya, Mkurugenzi na Balaza la Madiwani wa Halmashauri ya
wilaya ya Chunya.
Lengo kuu la kuanzishwa kwa
Tanzanite City ni kujenga uwezo wa taifa letu kwenye mambo ya teknolojia na
kuhamasisha mapinduzi ya viwanda yatakayoifanya Tanzania kuwa kiwanda cha
Afrika na kitovu cha ubunifu katika ukanda huu wa Afrika kusini mwa jangwa la
Sahara.
Jiji hili litasaidia kuwajengea uwezo wa ubunifu katika maswala
teknolojia, vijana wanaomaliza vyuo katika fani za sayansi na teknolojia, na
kuwawezesha kuanzisha viwanda na kuunda makampuni watakayo yaendesha kwa ubia
na wanachi wengine, kupitia klabu ya marafiki wa Tanzanite City
BAADHI YA CHANGAMOTO TUNAZOKWENDA KUZIJIBU
Kama
tujuavyo serikali yaawamu ya tano ya Mh.
John Pombe Magufuli imedhamiria kuipeleka Tanzania kwenye uchumi wa viwanda,
Lakini katika safari hiyo kuna changamoto kadhaa ambazo ni lazima zifanyiwe kazi.
· Mazingira magumu na
yasiyo rafiki yanayoyoua utamaduni wa kuwekeza katika
viwanda yanawafanya watanzania wengi kuagiza bidhaa za viwanda toka nje,
· Kukosekana kwa
kiunganishi kati ya wanjasiriamali wazawa na wawekezaji wa nje kunakotokana na tofauti kubwa sana katika technoljia. Tofauti hii
imefanya kuwa vigumu sana kwa wazawa kuweza kuhamisha teknolojia toka ng’ambo
hivyo kudumaza kabisa uwezo wetu na kutufanya tuendelee kuwa tegemezi
· Kukosekana kwa
mikakati sahihi ya kukuza na kuendeleza teknolojia ambayo
imefanya Kushindwa kubadli mafanikio ya tafiti kuwa viwanda (industrialization
of applied research); kushindwa kugeuza viwanda kuwa fursa za kibishara ambako
ndiko pesa ilipo.
SULUHISHO LETU
Ili
kujibu changamoto hizo, jiji la Tanzanite City limeanzishiwa kwa lengo la
kuweka mazingira bora ya kukuzwa ubunifu na kuanzishwa kwa viwanda na
makampuni. MAMBO SITA MUHIMU YATAKAYOFANYWA
NA TANZANITE CITY
1. Miundombinu bora (infrastructures
and sound facilities)
2.
Mikakati mahususi ya kukuza
vipaji na ubunifu
3.
Upatikanaji wa mitaji na
fedha
4.
Upatikanaji wa huduma
mbalimbali
5.
Kujenga mfumo madhubuti wa
biashara (Adequate business systems);
6.
Kutangaza na kukuza taasisi
za wajasiliamali na ujasiliamali (Promotion of SMIEs and entrepreneurship);
JIJI LITAKAVYOFANYA KAZI
Watu
wenye vipaji toka kokote kule duniani wataalikwa kushirikiana na vijana wetu
wataalam katika fani za Sayansi na teknolojia wanaohitimu vyuo ambao watawekwa
kwenye makambi ya teknlojia (classified technology development camps), katika jiji hili ili waweze kubuni na kujenga
uwezo wa kutengeneza bidhaa mbalimbali za kitechnolojia huku wakipewa kila aina
ya msaada watakaohitaji, kuanzisha viwanda pamoja na kuanzisha makampuni
watakayoyamiliki kwa ushirika na watanzania wengine kupititia Klabu ya marafiki
wa Tanzanite City.
Vijana hawa wataalam
watapewa mission mahususi za kubuni na kujenga uweza wa kuzalisha teknlojia
kulingana na vipaumbele na mahitaji soko, kukopi teknolojia ambazo tayari zipo,
kuzifanyia maboresho kulingana na mahitaji ya soko, na kuanzisha bidhaa na
teknoljia mpya ambazo ni zetu wenyewe baada ya kuwa tumejenga uwezo wa kutosha.
Lengo ni kujenga
uwezo wetu wa ndani wa kuzalisha bidhaa za kiviwanda na kiteknoljia, kwa mfano
badala ya kuuza simu toka nchi za Asia, tuunda na kuuza simu zetu wenyewe!
Badala ya kuifuata Guangzhou kule Uchina tunataka kujenga Guangzhou yetu hapa
hapa nchini
TUNAHITAJI NINI TOKA KWAKO MDAU
Tunawataka
wanachi na wadau wengine kujiunga na
klabu ili;
Kwanza waweze
kuchangia kwenye ujenzi wa jiji kwa
fedha au mawazo
Pili waweze kushiriki
kikamilifu kwenye ujenzi wa Tanzania mpya
Wewe kama mdau muhimu
tunakuaomba tuungane na Mh Rais John Pombe Magufuli na mkuu wetu wa Mkoa ambaye
pamoja , Wabunge wetu katkia juhudi zao za kuleta maendeleo ya Viwanda na
kukuza uchumi wa Mkoa wetu .
TUMEDHARIA
KUIFANYA MBEYA KUWA GUANGZHOU YA AFRIKA,
Tanzanite City Chunya Full Council Briefing Part 1
Sehemu ya kwanza ya mkutano wa utambulisho wa Tanzanite City kwa wakuu wa idara na madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Chunya ambako ndiko jiji linajengwa.
Sunday, October 8, 2017
TANZANITE CITY YASHIRIKI VILIVYO KATIKA JUKWAA LA UWEKEZAJI MBEYA
Salaam za pongezi kwa Mh. Dr. Mary Mwanjelwa (Naibu Waziri Mteule wa Kilimo)
![]() |
| Mheshimiwa Dr. Mary Mwanjelwa, Naibu Waziri Mteule Wa Kilimo |
Kamati
ya uongozi inayoshugulikia ujenzi wa jiji la sayansi, teknolojia na ubunifu la
Tanzanite City – Chunya, pamoja na wadau wetu wote kupitia klabu ya marafiki wa
Tanzanite City, tunapenda kutoa pongezi zetu za dhati kabisa kwa mbunge wetu wa
Mbeya na mdau wa Tanzanite City, Mheshimiwa Dr. MARY MWANJELWA kwa kuteuliwa
kwake na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. John Pombe Magufuli Kuwa
Naibu Waziri wa Kilimo.
Tunatambua
uwezo mkubwa sana alionao Mh. Mwanjelwa katika kutekeleza majukumu yake. Sisi kama
wadau wa maendeleo ya viwanda na Teknolojia tunatambua jukumu kubwa na zito
analokwenda kulibeba Mh Mwanjelwa, si mchezo-mchezo bali anatakiwa kuwa mbunifu
sana na asiyechoka kujifunza. Nchi yetu ni kubwa sana na ina matatizo mengi mno
yanayohusiana na wizara anayokwenda kuifanyia kazi.
Moja
ya changamoto ambazo Mh. Naibu Waziri atakutana nazo katika utekelezaji wa
majukumu yake ni matumizi duni ya teknolojia katika kilimo kwa ujumla wake na namna
ya kuongeza thamani ya mazao ya kilimo. Katika wakati huu ambao taifa letu lipo
kwenye kipindi cha mpito kuelekea uchumi wa kiviwanda, suala la teknolojia
linapaswa kupewa kipaumbele kwani linagusa kila Nyanja ya kilimo, kuanzia
kwenye maandalizi ya ardhi ikiwa ni pamoja na kuilima, kupanda na kupandikiza
mazao mashambani, kutunza mazao yaliyoshambani ili yaweze kutoa matunda bora na
ya kutosha, uvunaji wa mazao na kuyasafirisha toka mashambani, uhifadhi wa
mazao ghafi ya kilimo pamoja na kuyaongezea thamani. Yote hayo yanahitaji
teknolojia kwa mapana yake!
Mh.
Naibu Waziri, ni vigumu sana kuweza kuendelea kama taifa, iwe ni kwenye kilimo,
viwanda au hata biashara tu, iwapo tutapuuza matumizi ya teknolojia. Lakini pamoja
na kutilia maanani matumizi hayo ya teknolojia, bado hatutaweza kufikia malengo
yetu ya kiuchumi kama tutaendelea kuwa tegemezi kwa kiteknolojia toka nje. Kwani
hao tunaowategemea wao pia wanavyo viapaumbele vyao ambavyo siyo lazima
vifanane na vyetu. Hivyo sasa ni jukumu letu kama kweli tunataka kwenda kwenye
uchumi wa kati, wa viwanda na kilimo cha kibiashara na chenye tija, kuanza sasa
kujenga uwezo wetu wenyewe kwenye mambo ya technolojia ambao ndiyo mhimili wa
hivyo viwanda na hicho kilimo tunachokitaka.
Mh.
Naibu Waziri, sisi tumeanza na Tanzanite City, ni safari ngumu na ndefu, lakini
tumedhamiria kufika mwisho, tunaamini kuwa, kwa kuwekeza kwenye vipaji vya
vijana wetu, na kuwasaidia kutimiza ndoto zao, tutabadilisha mustakabari wa
taifa letu na kuboresha sana kilimo chetu, tukishirikiana sisi wanachi, wadau
wa maendeleo, pamoja na serikali tunaweza kuifanya Tanzania kuwa kiwanda cha
Afrika, na kitovu cha ubunifu katika maswala ya teknolojia.
Mh.
Naibu Waziri, tuna jua NIA UNAYO, SABABU UNAYO NA UWEZO UNAO! Tunakuahidi ushirikiano
wetu, tunakuombea afya njema, hekima, na heshima kwa watu unaowaongoza, wengi
wamepita na hawajaacha alama yoyote baada ya wao kuondoka, na wewe hutaishi
milele kwenye hiyo nafasi, lakini tunatamani kuona alama za kazi zako zikidumu
daima kwa vizazi vingi vijavyo!! TUNAJUA NA TUNAAMINI UNAWEZA!!! Tuna kutakia
kila lililo la heri, ufanikiwa katika majukumu yako hayo kwa taifa letu, MUNGU
Akubariki na akulinde siku zote za maisha yako. Amina.
Wednesday, August 2, 2017
Monday, November 21, 2016
LETTER TO HIS EXCELLENCY PRESIDENT DR. JOHN POMBE MAGUFULI
Dear Mr. President,
ESTA-TZ Limited is dealing with the development of a city of science, technology and innovation, I.e. ESTA-Tanzanite City. The City is our endeavor to stimulate the development of home grown technology capabilities by empowering and enabling university and college graduates in the fields of science and technology, to develop technology and manufacturing capabilities, then assist them to launch and build new technology-based industries that will be owned in partnership with other citizen through Friend’s Club of the Tanzanite City
ESTA-TZ Limited is dealing with the development of a city of science, technology and innovation, I.e. ESTA-Tanzanite City. The City is our endeavor to stimulate the development of home grown technology capabilities by empowering and enabling university and college graduates in the fields of science and technology, to develop technology and manufacturing capabilities, then assist them to launch and build new technology-based industries that will be owned in partnership with other citizen through Friend’s Club of the Tanzanite City
Our
motivation being to make the city an Africa’s factory and innovation
powerhouse, that will affect everyone’s life in this continent and play great
role in improving the quality of life, economic growth and protecting our
environment, the Tanzanite City, will be the mining of the talents from the brains of our young
people and a factory for processing them out into automobiles, ships,
computers, processing industries, TVs, mobile phones, etc. it will be the hatchery of technology industries in Tanzania,
Knowing
that this is very big undertaking that we can only achieve with the assistance
and generosity from all members of our community, the government and
non-government Institutions, and that Without these, achieving this mission
will not be possible, we are now working to establish a Not for Profit Trust
(ESTA-Tanzanite City Trust) that will be responsible to support the whole
mission as described in the Grand Concept Manual
Dear
Mr. President, with this letter first of all I would like to recognize your effort
to transform our country especially with your ambition to make Tanzania highly
industrialized in the next ten years. We know how tuff it is to change the mindset
of the people and make them believe in what you are doing against their status
quo, don’t be discouraged, one day if not now people will understand your
language and see what you are looking after, but before we reach there be sure
that a lot will happen to either encourage or discourage you. All in all, it
needs big heart and a lot sacrifices that already you have demonstrated, we are
sure with that spirit of yours we are heading the right direction.
Dear
Mr. President, during Mwl. Nyerere’s age, at schools we were taught that for
our nation to develop we need four major ingredients; Land, good politics,
people and good governance. With changes that had occurred in the world since
the end of cold war in the end of 1980s we can now redefine the ingredients of
development as; Good governance, technology and nature resources. Good
governance is mandatory but must be mixed with either of the two, technology or
access to natural resources or both as it is for the highly developed
countries. The poorest countries have only one ingredient and they have stuck,
fast developing countries have at least two, good governance and technology, or
good governance and plenty of natural resources.
Good
governance puts the systems in place and brings discipline and makes the people
focus on development businesses. Where good governance is blended with
technology, the country becomes strong and stable and can access natural
resources from other countries. And when the good governance is blended with
plenty of natural resources, the countries could properly plan the use of their
resources to acquire the technology they need. Having technology or natural
resources without good governance normally leads to the violence and unrests
caused by scrambles for control among the greedy
Dear
Mr. President, you are now transforming our nation towards good governance and
discipline, blending it with the plenty of natural resources our country have
been endowed, we only need technology to move from where we are to our promise
land. With technology, we will be able to sustainably harvest our natural
resources, process them and utilize them to bring wealth to our people, with
technology we can make our country the Africa Factory where all other African
countries will turn to for their various needs instead of going all the way out
to other continents. This will be great footstep embracing the dream of the
father of our nation of uniting Africa economically
As I
have said above, this is a tuff undertaking and required the participation of
all stake holders and citizens of this country to make it. You my president
alone won’t succeed, you need our support, and your government if they real
want to support your vision of industrialized Tanzania, must truly commit
themselves to work with big dreamers who have great ideas and want to change
this world.
We at
ESTA-TZ believe that this country will be developed by our own efforts, our
brains and determinations, no one will come from china, from Europe, from Asia
or from America to develop us but all of them can render great contribution to
our development if we will be able to partner with them and benefit from each
other, they need our resources as much as we need their technology, let’s play
the right card now for the better future of our nation.
Understanding
this all, the Tanzanite City is one of the strategy that will provide sound
facilities & infrastructures required to cater the needs of the expected
scientific and technological advancement and supporting R&D and other
technological operations in the Tanzanite City and provide to the talents and
experts, the required resources to support their’ activities and enable them to
conduct researches, build new instruments, conduct experiments, and
scientifically test their ideas in development of technologies that address
social and economic needs of our people, and bridge the gap between need and
means; between scientific & engineering challenges and technological
innovations needed to overcome them; between laboratory development and
demonstration in the field.
To solve our
problems and develop the capability to create jobs and increase the flow of
foreign currencies into our country, we must greatly reduce our dependence on
imported items and instead we should develop the technology capability to
manufacture industrial items to carter our own needs and the needs of our
neighboring countries, In order to achieve
this. The Tanzanite city if successful will address the following
issues:
Importing everything while we export less: This not only narrows the opportunity of our nation to create
jobs but also drains our foreign currency reserves which by the way we don’t
have much because we don’t export much as we import, to combat this, we must continuously
and sustainably reduce within specific period of time, our dependence to the
import of technology items by developing technology capabilities to
manufacturing of our own products rather than selling products from other
countries.
Utilized our country’s geographical position to our advantage: Our country is a gate way by which our land locked neighboring
countries use for import of their industrial items and exports of raw
materials. When they pass by, we join them and go all the way out there to
bring things that our young graduates from our universities would have been
manufacturing here.
Export of raw materials: Since
we do not have technologies for processing our agricultural products and
mineral raw materials we export them raw, our neighbors are also using our
country to export their raw materials. The question is wouldn’t it be wealth if
we could process those materials into finished or semi-finished products before
we allow them out of our boarders? What does it take and How do we manage?
Where and When should we start? how do we start?
Lack of access to the new technologies & mechanisms for
technology transfer: Now our countries are in
competition to lure the foreign investors (FDI) to invest in various
manufacturing sectors such as assembling and processing industries. But due to
the fact that there is big gap in technology capabilities between the foreign
investors and our entrepreneurs and the link between them is very weak, it is
difficult for our entrepreneurs gaining access to the new technologies via
foreign joint ventures and Foreign Direct Investment hence they are unable to
absorb, assimilate, and innovate the new technologies
Because
our country has no plenty of resources to facilitate quick evolution
industrialization, the best way to go about may involve doing the following:
·
develop our own homegrown
technology capabilities and promote rapid progress of export-oriented
industrialization and development of strong and competitive Small & Medium
Industrial Enterprises as an essential prerequisite for continued development
and increased competitiveness of the manufacturing industries.
·
creating geographical proximity
between the core industries and its upstream and downstream businesses to easy
sharing of the common facilities and resources hence reducing technology
development and manufacturing costs, we should create perfect ecosystem and
link between economic development, people development and government revenue
creation,
·
creating link between foreign
investors especially assembly industries and local entrepreneurs especially
supporting industries and facilitate innovation driven growth of
technology-based industries and finally We need to create conducive environment
for launching and building myriad technology-based industries and nurture them
through to stand-alone stage, and connect them with foreign investors to create
partnership that will benefit both
And
that is all about development of the Tanzanite City of Science, Technology and
Innovation
Dear
Mr. President, May I Take this Opportunity to ask your government to support us
and join hands with us to achieving this crucial mission. The generous support of
your government will make it possible to develop our own “Guangzhou”, where
people from other African countries will turn to for their shopping instead of
just passing by and going all the way to Asia buying items that we could
manufacture here so creating jobs and increasing our foreign currencies
reserve.
From
your government, we need two things; number one is land - about 400sqkm with
expansion provision for the development of the city where about 100,000
industrial enterprises will be built in the next 15 year that will create about
two million direct jobs in this city. Second is support from your governments
institution such as COSTECH, TIRDO, SIDO, BRELA, TFDA, TBS etc.
With
this support, we are sure to TURN BUSHES INTO HIGHLY INDUSTIALISED CITY, and
make our own GUANGZHOU & SILICON VALLEY for Africa
Regards
Nsollo Nkalla
CEO & Founder
ESTA-Tanzanite City
0713253250 / 0752229090
Subscribe to:
Posts (Atom)





